Shirikisho la Wakuu wa Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume kwa upande wa wanaume
nchini Tanzania katika mkutano wake mkuu wa mwaka uliofanyika Jimboni Morogoro, umewachagua
wafuatao kuongoza RSAT kwa kipindi cha miaka miwili, yaani kuanzia Juni 2013 hadi
Juni 2015.
Waliochaguliwa ni kama ifuatavyo: Mwenyekiti ni Padre Shukrani
Kasian Mbirigenda, wa Shirika la Wakamiliani. Mwenyekiti Msaidizi: Padre Reginald
Mrosso, Wamissionari wa damu Azizi ya Yesu Wajumbe: Br. Valeriani Mchome: Mabruda
wa Yesu mchungaji mwema, Same Mjumbe: Br. Venance Kapita, Mabruda wa Upendo, Kigoma Mjumbe:
Padre Wolfgan Pisa, Wakapuchini.
Taarifa hii imetolewa na Mheshimiwa Padre
Firmati Tarimo, IC, Mwenyekiti aliyemaliza muda wake RSAT.