Papa akutana na watetezi wa haki msingi za binadamu kutoka Argentina
Baba Mtakatifu Francisko, Jumatatu, tarehe 24 Juni 2013 amekutana na kuzungumza na
Bwana Adolfo Pèrez Esquivel, Mshindi wa Tuzo ya Amani mjini Vatican, aliyekuwa ameambatana
na Bwana Felix Diaz, mkuu wa Kabila la Qom lililoko nchini Argentina pamoja na ujumbe
wao!
Viongozi hao wamemshukuru na kumpongeza Baba Mtakatifu kwa kuwapatia
fursa ya kuzungumza nao pamoja na jitihada zake za kuwalinda na kuwatetea wazawa wa
Argentina na Amerika ya Kusini katika ujumla wake. Viongozi hao wanasema, wanaguswa
sana na uvunjifu wa haki msingi za binadamu wanazofanyiwa wazawa wa Argentina na Amerika
ya Kusini katika ujumla wao hasa kuhusiana na utambulizo na ardhi yao!
Taarifa
hii imetolewa na Padre Federico Lombardi, msemaji mkuu wa Vatican.