2013-06-22 14:21:18

Ninyi ni Wachungaji mliombeba Kristu ndani mwenu- Papa.


Ninyi ni wajumbe wa kumpeleka Kristu ulimwenguni. Na kamwe msisahau kwamba ninyi ni wachungaji, mnao mwasilisha Kristu ulimwenguni, mkiwa watu mlio achana na roho wa kipebari na maisha ya kidunia ambamo mna hatari ya kukebehi hata utume Mtakatifu wa kuwa mwakilishi wa Papa .

Papa Fransisko , alitoa ujumbe huo kwa Mamia ya wawakilishi wa Papa ambao pia wanajulikana kwa jina la Wajumbe wa Kitume au Manusio, ambao katika ujumla wao wote wamekusanyika Vatican toka pande zote za dunia, kwa ajili ya mkutano kisala na tafakari kwa muda wa siku mbili, katika mtazamo wa Mwaka ya Imani.

Akiwahutubia siku ya Ijumaa, Baba Mtakatifu Fransisko, aliangalisha katika Mwaka wa Imani . Na mwanzo alitoa shukurani zake za dhati kwa Bwana kwa majaliwa yake ya kuwakusanya pamoja na katika muda huu w siku mbili wa tafakari na sala, wakiwa wmashikamana pamoja katika hali ya udugu na umoja chini ya Kiti cha Petro na Askofu wa Roma. . Na aliwashkuru wote kwa maneno mazuri yaliyotolewa na Kardinali Bertone, kwa niaba yao wote, na kwa huduma yao nzuri, wanayo itoa kwa niaba yake na kwa niaba ya kanisa zima katika utume wa umoja na Khalifa Mtume Petro,akisema, na hivyo ni wawakilishi wake katika makanisa yaliyotwanyika duniani kote na kwa serikali na katika maana ya kutoa sura ukatoliki wa Kanisa la ulimwengu .

Papa , ameonyesha kutambua kwamba, maisha ya Nunsio , ni maisha ya kuhamahama , toka sehemu moja hadi nyingine, bara hadi bara, taifa hadi taifa na ndivyo wanavyobadilisha hali halisi za maisha ya kikanisa, na aliwashukuru kwa kukubaliana na hilo na kuweza kuyaishi maisha hayo. Papa ameyataja maisha hayo, kwmba huotoa picha msafiri, katika mtazamo wa kina wa maisha ya imani, kama ilivyokuwa kwa Ibrahimu, mtu wa imani katika safari: Mungu alimtaka aondoke nchi yake, na kuayaachamazingira aliyoyazoea na kuanza mwendo kwa kuamini ahadi ya Mungu . Na aliendelea kuwa namtu wa imani na tumaini , kama ilivyoandikwa kaitak kitabu cha Mwanzo.

Papa alieleza na kutaja kwamba kuna orodha ya mifano ya mingi ya Mababa wa Imani walioiingigia safari hii ya imani na kuona matokeo ya ahadi ya Mungu. Maisha kama hayo yana thamani kubwa , na ni maisha kama yao , pale wanapo yaishi kwa upendo mkuu na wa kina na kwa kumbukumbu za wito wao wa kwanza .

Pia aliendelea kutafakari juu ya kuona mbali , akiitazama tena mifano mingi iliyoandikwa katika Agano la Kale na kuwahimiza Mabalozi wa Papa kuwa na mtazamo huo kama msingi wa msukumo wa ndani, wa unao toa nguvu za kusonga mbele kumtafuta Kristu, , ambaye ndiye ahadi yetu.

Na aliwarejesha katika barua maarufu ya Aprili 25, 1951, hotuba ya aliyekuwa Katibu Mbadala wa Nchi kwa wakati huo, , Monsignor Montini, iliyomzungumzia maana ya kuwa mwakilishi wa Papa, kwamba, ni yule mwenye kuwa na ufahamu wa kweli kwamba, ndani mwake yu pamoja na Kristu kama hazina ya thamani anayotakiwa kuiwasilisha kwa watu. Kujenga mahusiano ya karibu na Yesu Kristo lazima iwe kula chakula cha Krsitu kila siku, kwa sababu ni katika chakula hicho, ndicho kinawarejesha daima, katika kumbukumbu ya kwanza ya kukutana na Kristu, na pia kwa sababu ni kielelezo za uaminifu cha kila siku katika wito wao. Kuwa karibu na Kristu katika sala , maadhimisho ya Ekaristi, katika huduma ya upendo.


Papa pia aliwaasa Mabalozi juu ya hatari YA kusalimisha wito wao kwa roho wa kupenda dunia: kujisalimisha katika roho wa malimwengu, ambayo hatua kwa hatua huongoza katika ubinafsi , kiburi na majivuno. Huko humwondoa mtu katika kuwa mtumishi kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Papa aliwaasa juu ya aina ya "roho huyo wa ubepari na maisha ya starehe ambayo hatima yake huwa ni majuto. Na pia alionya juu ya roho huyo wa kidunia anayejificha ndani , hata wakati mwingine hujenga roho wa kejeli ,unafiki na usaliti , kwa wanaonekana kukubaliana na wengine lakini kumbe kuna tabia ya kukosoa wengine nyuma ya migongo ya wenzao.

Papa aliwakumbusha Mabalozi hao, wasisahau utume wao wa kwanza ni kuwa ni Wachungaji. Wao ni wawakilishi wa Papa , wawakilishi wa upendo wa Kristu, wawakilishi wa kikuhani kama wachungaji, ingawa si kama maaskofu wa eneo fulani au viongozi wa mtaa fulani wa Kanisa, lakini ninyi ni Wachungaji wanaotumikia Kanisa, wahamasishaji na wahudumu wa usharika,kazi ambao si rahisi na yenyekudai majitoleo , na daima yenye kuhitaji kumulikiwa na upendo wa kina! Hata katika mahusiano na Mamlaka za Kiraia na Wale wanaowasaidia bado ni ninyi ni wachungaji , wanaotakiwa daima kutafuta mazuri kwa ajili ya wote , mema ya Kanisa na ya kila mtu, alisisitiza Papa .

Papa alihitimisha hotuba yake kwa kuwataka Mabalozi hao , kuivaa roho ya upole, uvumilivu na huruma; wakihamasihswa na umaskini wa ndani na uhuru wa Bwana na pia na kuwa wanyenyekevu katika wa maisha, bila ya kutafuta makuu, wakijiepusha na tamaa na ubabe wa madaraka. Wajione kuishi kw aunyenyekevu wa kuwa wachumba wa Kanisa la Kristu.. wakwia wamevalishwa uwezo wa kulichunga kundi la kondoo waliodhaminishwa kwao. Kulitunza na kudumisha tumaini la nuru ya wokovu katika mioyo yao, kwa upendo na uvumilivu, na kwa msaada wa kudra ya Mungu kwa watu wake. Papa alieleza kwa kuwatazamisha katika mfano wa maisha ya familia Takatifu, jinsi Mt. Yosef, alivyomtunza Maria na Yesu.

Na aliwakaribisha kuendelea kutafakari juu ya huduma yao muhimu na ya thamani kubwa kwa Kanisa lote,a ktika mtazamo kwamba, maisha yao ni hija ya kuendelea kutembea bila ukomo wa kuwa na kituo kimoja cha kutulia kwa muda mrefu sehemu moja, au katika utamaduni mmoja, au katika hali halisi maalum za kikanisa. Ni maisha kwenye barabara kutembea daima na Yesu Kristo mwenyewe aliye wabariki kwa mkono wake.








All the contents on this site are copyrighted ©.