Weka hazina moyoni na si katika ghala la kidunia- Papa
Kumwomba Mungu Neema ya kuwa na moyo wa kujua kupenda , ni kujiwekea hazina moyoni.
Papa Fransisko , alieleza wakati wa Ibada ya Misa mapema Ijumaa asubuhi katika Kanisa
dogo la Mtakatifu Marta mjini Vatican.
Ibada aliiongoza akisaidiana na Kardinali
Fransisko Coccopalmerio, pamoja na Askofu Juan Ignacio Arrieta na José Aparecido
Gonzalves de Almeida, ambao ni rais, katibu na Katibu mwandamizi wa Baraza la Kipapa
kwa ajili ya Maandiko ya Kisheria. Walikuwepo pia baadhi ya wafanyakazi wa idara
za baraza hilo, na wafanyakazi wa kiwanda binafsi cha Kanisa Kuu la Yohane wa Laterano
, wakiongozwa na Msgr. James Ceretto, na wafanyakazi wengine katika jengo la Domus
Sanctae Marthae.
Papa alieleza jitihada za kuiwinda hazina hii, ambayo ina
nguvu za kutupeleka pia katika maisha ya baadaye, baada ya maisha haya ya kawaida,
ambayo ndiyo dhamira ya Mkristo. Daima kuwa na hazina hii, kama Yesu alivyowaambia
wafuasi wake, kama iivyoandikwa katika kifungu cha Injili ya Mathayo: "mahali
ilipo hazina yako, ndipo pia yalipo mapenzi ya moyo wako. Papa ameeleza na kubaini
hatari iliyopo ya kuchanganya hazina hii na hazina za kidunia zidanganyazo ambazo
Mkristu ni lazima kuziambua na kujiweka mbali nazo , ambazo hulindikana wakati wa
maisha lakini hutoweka mara baada ya kifo kutokea.
Papa alieleza, na kutoa
mfano kwamba , katika maisha yake hajawahi kuona, mali ya marehemu ikiandamana hadi
kaburini “Sijawahi kuona lori, mali ya marehemu ikiandamanishwa katika msafara wa
maziko ili ikazikwa na marehemu. Lakini utajiri wa kiroho huandamana na mtu hadi
kaburini. Hakuna anayeweza kuipokonya toka wka mmliki , hivyo mtu huzikwa nayo na
kuendelea kuwa nayo katika maisha ya milele.
Hazina hii ya kiroho, pia tunaweza
kuitoa pia kwa watu wengine na kwetu isipungue kitu. Hazina hii inakuwa ni sifa yetu
na haki yetu yakuwa na Yesu ndani mwetu. Na hiyo ndiyo tunayotakiwa kuibeba muda
wote. Na ndiyo tunatakiwa kuipeleka kwa wengine, nayo ni hazina ya upendo , huduma,
uvumilivu, wema na huruma. Ni hazina nzuri ya kuihifadhi moyoni muda wote alisisitiza
Papa Fransisko.
Kwa hiyo, kama ilivyoandikwa katika Injili , Papa aliendelea
, hazina ya thamani machoni pa Mungu, ambayo tunajikusanyia hapa dunia na pia hukusanywa
mbinguni kwa ajili yetu. Papa alieleza na kuonya juu ya utafutaji wa hazina zinazotuweka
mbali na Bwana. Hazina zinazohaingaisha na kuuchosha moyo , kufikiria tu juu ya mali
za kidunia zisizorithisha moyo. Wakati kuitafuta hazina ya upendo unaotajwa na Kristu
huutuliza moyo na kufarijika hata kimwili. Katika hatua hii, anasema Papa Francisko
, Kristo amelitaja “jicho", ambayo ni ishara ya "nia ya moyoni" na yale yanayo
jitokeza kimwili kwamba , moyo wa upendo huangazia nuru mwili, na moyo mbaya, huupeleka
mwili gizani. Papa aliomba maombezi ya Mtakatifu Luigi Gonzaga aliyekumbukwa na
Kanisa leo, ili Bwana atujalie neema ya moyo mpya,"moyo wa nyama":