Kristo ndiye anayeliongoza Kanisa lake ili liweze kuzaa matunda ajaa!
Wakati huu ambapo waamini bado wanamshukuru Mwenyezi Mungu kwa moyo wa ujasiri, hekima
na busara ulioneshwa na Baba Mtakatifu mstaafu Benedikto wa kumi na sita kwa kung'atuka
kutoka madarakani kwa uhuru na utashi kamili na hatimaye, kuchaguliwa kwa Papa Francisko;
Yeye mwenyewe anapenda kuwakumbusha watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, Yesu
ndiye anayeliongoza Kanisa. Ndiye anayefanikisha utume na shughuli mbali mbali za
kichungaji!