Jumatatu Papa alikutana na Rais wa Venezuela , Mheshmiwa Nicolas Maduro. Mkutano
wao ulilega zaidi masuala ya kijamii na kisiasa kulingana na hali halisi za taifa
hilo, hasa baada ya kifo cha Rais aliyependwa sana na watu Hugo Chàvez, na pia juhdi
za kutokomeza ufukara na mapambano dhidi ya uhalifu na biashara haramu ya dawa za
kulevya . Wakuu pia walijadili, uwepo wa historia ya kanisa katika taifa la Venezuela,
na juhudi zake katika kuchagia utoaji wa elimu, huduma za afya na matendo mengine
ya huruma. Na waliona kuna haja ya kuwa na majadiliano ya kweli na thabiti mara kwa
mara kati ya Baraza la Maaskofu la Venezuela na serikali , kwa ajili ya ufanikishaji
haraka zaidi, maendeleo katika taifa lote. Na mwisho walilenga katika hali za kimkoa
katika mtazamo maalum wa amani kwa taifa lote la Venezuela. Mwisho wa mkutano
wao , Papa na Rais Maduro waliibadilishana zawadi.