Papa atoa wito: Semeni ndiyo kwa maisha na hapana kwa Kifo !
Papa Fransisko ametoa wito kwa watu wote kuyatetea maisha na hapana kwa kifo. Kusema
ndiyo kwa maisha na kukataa kila kitendo kinachotaka kukatisha uhai , kusema hapa
kubwa kwa kifo. Papa alitoa wito huu wakati wa hotuba yake siku ya Jumapili asubuhi,
ambamo Mama Kanisa aliadhimisha SIKu ya Injili ya Maisha “ Evangelium Vitae” .
Katika
homili yake aliyoitoa mbele ya umati wa watu wapatao 200,000 waliofurika katika
Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro , kuhudhuria Ibada ya Misa iliyoongozwa na
Papa, na pia kwa ajili ya sala Ya Malaika wa Bwana, ibada na sala zilizofanyika katika
mtazamo wa maadhimisho Mwaka wa Imani, siku ililega zaidi majitoleo ya Injili ya
Maisha.
Katika homilia yake , Papa Francis, alitafakari Maandiko Matakatifu
yanavyotuambia mara kwa mara, jinsi Mungu Mmoja Hai, ndiye mwenye kutoa maisha.
Hata
hivyo, alisema kwamba "mara nyingi, watu hawachagui maisha, hawaikubali Injili ya
Maisha bali hujiachia wenyewe kuongozwa na itikadi na njia yapotofu katika kufikiri,
zenye kuwekea maisha kibambaza, njia zisizo heshimu maisha, kwa sababu wamekubali
kuongozwa na nguvu za ubinafsi katika utafutaji wa maslahi faida, mamlaka na kujijifurahisha
, na si kwa ajili ya upendo kwa wengine , au kujali manufaa ya wengine.
Baba
Mtakatifu aliendelea kusema kuwa, watu wana ndoto za kujenga upya "Mnara wa Babeli",
mji wa mtu asiyekuwa na Mungu. Wanaamini kwamba kumkataa Mungu, kuukataa ujumbe wa
Kristo na Injili ya Maisha, huwaongoza kwa namna fulani katika furaha, kuwa na uhuru
kamili wa kutimiza malengo yao ya kibinadamu. Na kama Kama matokeo yake , Papa aliendelea,
Mungu aliye hai huondolewa na badala yake huwekwa miungu mbadala mfululizo ya kibinadamu
ambayo hulewesha mtu katika uhuru bandia , ambao mwisho wake hujenga aina mpya za
mfumo wa utumwa na kifo.
Papa alimalizia homilia yake na wito kwa waamini,
kuyaonamadhara hayo ni hivyo waseme Ndiyo kwa Mungu ambaye ni Upendo. Ndiyo kwa Maisha
ya kushikamana na Mungu ndiye uhuru wa kweli na hamfadhaishi mtu. Mara baada ya
Ibada ya misa Takatifu, Papa aliongoza sala ya Malaika wa Bwana. Katika hotuba yake
fupi, Papa alielekeza mawazo yake katika mifano ya watu walioyatetea maisha kikamilifu,
akiangalisha katika tukio la Siku ya Jumamosi ambamo Mama Kanisa alimtagaza kuwa
Mwenye Heri , baba wa watoto saba wa Capri Italy, aliyeuawa katika kambi za msongamano
za Nazi mwaka 1944, ambaye aliyaokoa maisha mengi katika kambi hiyo , kabla ya kupoteza
yake mwenyewe.
Papa pia aliitumia nafasi hiyo kusalimia washiriki wa Mkutano
wa hadhara wa wanachama wa Harley-Davidson, kwa ajili ya kutumia kwa miaka 110,
tangu kutengenezwa kwa pikipiki, yenye nembo hiyo ya Harley Davidson, ambayo inajulikana
kuwa aina ya kipekee na mashuhuri Marekani. Kwa ajili ya sherehe hii zaidi ya wapanda
pikipiki 100,000, walikusanyika mjini Roma mwishoni mwa wiki hii. Kati yao 1400
wakiwa na pikipiki zao , walibarikiwa na Papa wakati huo wa sala ya Malaika wa Bwana.