2013-06-15 10:02:12

Mkutano wa G8 na Uwakilishi wa Bara la Afrika


Rais Jakaya Mrisho Kikwete amealikwa kuiwakilisha Tanzania na Afrika katika shughuli za Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Nchi Zenye Viwanda Vingi Duniani – G8 wa mwaka huu unaofanyika London, Uingereza. Rais Kikwete ambaye pia alihudhuria mkutano wa mwaka jana wa G-8 Marekani kwa mwaliko wa Rais Barack Obama, amealikwa na Waziri Mkuu wa Uingereza, Bwana David Cameron kuhudhuria mkutano wa mwaka huu.

Rais Kikwete ambaye atashiriki katika kikao cha kujadili ukuaji wa uchumi ataungana na Rais John Mahama wa Ghana, Rais Alpha Conte wa Guinea, Rais Hassan Sheikh Mahmound wa Somalia na Rais Blaise Compaor’e wa Burkina Faso kushiriki katika kikao hicho. Rais Kikwete ameandamana na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna Tibaijuka na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo.








All the contents on this site are copyrighted ©.