2013-06-13 15:43:24

Waziri mkuu wa Slovenia akutana na kuzungumza na Papa Francisko mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko, Alhamisi tarehe 13 Juni 2013 amekutana na kuzungumza na Bi Alenka Bratusek, Waziri mkuu wa Slovenia na ujumbe wake, waliomtembelea mjini Vatican. Waziri mkuu baadaye alipata fursa ya kukutana na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican pamoja na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Baba Mtakatifu na mgeni wake wamejadili pamoja na mambo mengine uhusiano uliopo kati ya Vatican na Slovenia na kwamba, wameonesha utashi wa kuendeleza ushirikiano huu kwa ajili ya mafao na ustawi wa Kanisa na Jamii kwa ujumla wake. Wamekubaliana kimsingi kuhusu mchango mkubwa ambao umetolewa na Kanisa Katoliki nchini humo pamoja na kudumisha uhuru wa kuabudu kwa ajili ya amani, utulivu na maendeleo ya wananchi wa Slovenia.

Wamegusia pia changamoto zinazoikabili nchi hiyo kwa sasa na mchango ambao Kanisa linaweza kutoa katika sekta ya elimu na afya. Masuala ya kimataifa yamejadiliwa pia na viongozi hawa wawili.







All the contents on this site are copyrighted ©.