2013-06-11 08:26:22

Serikali inapaswa kulinda na kudumisha haki msingi za raia wake ili kuendeleza amani na utulivu!


Askofu mkuu Paul Ruzoka, Mwenyekiti wa Tume ya Haki na Amani, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mahojiano na Radio Vatican anabainisha kwamba, mchakato wa majadiliano ya kidini katika kujenga, kulinda na kudumisha misingi ya haki, amani na utulivu nchini Tanzania unapaswa kusimamiwa vyema na Serikali yenyewe. RealAudioMP3

Askofu Ruzoka anasema kwamba, shida kubwa inayojitokeza kwa sasa ni kuangalia masuala mbali mbali ya uvunjifu wa misingi ya haki na amani kama kielelezo cha kinzani na misigano ya kidini nchini Tanzania, jambo ambali si kweli. Haki msingi za raia na usalama wa maisha ya raia na mali zao ni mambo yanayopaswa kupewa msukumo wa pekee na Serikali ili kudumisha misingi ua uatwala bora kwa kuhakikisha kwamba, haki ya kila raia inalindwa na amani ina tawala.

Masuala ya uvunjifu wa amani yaangaliwe zaidi katika misingi ya haki na kwamba, haki isipolindwa na kudumishwa kunaweza kutokea uvunjifu wa amani.







All the contents on this site are copyrighted ©.