2013-06-10 09:36:12

Mchango wa vyombo vya habari vya kikristo katika kuhamasisha haki, amani, upatanisho na haki Mashariki ya Kati


Warsha ya siku mbili iliyojadili kuhusu mchango wa vyombo vya habari vya Kikristo katika nchi za Kiarabu imehitimishwa hivi karibuni kwa kupewa changamoto ya kuendelea kutoa huduma ya haki, amani, upatanisho na haki msingi za binadamu. Warsha hii imehudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Makanisa kutoka Mashariki ya kati na Askofu mkuu Claudio Maria Celli, Rais wa Baraza la Kipapa la Mawasiliano ya Jamii alihudhuria pia.

Wajumbe kwa pamoja wameangalia mchango makini uliotolewa na vyombo vya habari vya kikristo katika mapambazuko ya mapinduzi ya Kiarabu na kwamba, bado kuna changamoto kubwa kwa waamini wa dini mbali mbali huko Mashariki ya kati kuishi kwa amani na utulivu; kwa kuheshimiana na kuthaminiana kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya wengi.








All the contents on this site are copyrighted ©.