2013-06-08 14:41:20

Rais Giorgio Napolitano akutana na Papa Francisko mjini Vatican


Baba Mtakatifu Francisko, Jumamosi tarehe 8 Juni 2013 amekutana na kuzungumza na Rais Giorgio Napolitano wa Italia pamoja na ujumbe wake, ambao baadaye walikutana na kuzungumza na Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican aliyekuwa ameambatana na Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa mjini Vatican.

Katika mazungumzo yao, viongozi hawa wawili wameridhishwa na uhusiano mwema uliopo kati ya Vatican na Italia. Wamejadili kwa kina na mapana hali ya Italia kwa sasa na mchango wa Kanisa Katoliki katika ustawi na maendeleo ya wananchi wa Italia. Wamegusia pia masuala ya kimataifa na kwa namna ya pekee, kinzani na migogoro ya kivita huko Mashariki ya Kati, Kaskazini mwa Afrika pamoja na madhulumu wanayokumbana nayo Wakristo katika nchi mbali mbali duniani.

Baba Mtakatifu na Rais Napolitano wameonesha utashi wa kuendelea kushirikiana kwa pamoja katika masuala ya kimataifa na kwa namna ya pekee, katika harakati za kulinda na kudumisha uhuru wa kidini.







All the contents on this site are copyrighted ©.