Mzee Madiba amelazwa tena! Hali yake inasemekana kuwa tete!
Mzee Nelson Mandela, Rais mstaafu wa Afrika ya Kusini, siku ya Jumamosi asubuhi amelazwa
tena baada ya hali yake kuanza kudhohofu kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa mapafu.
Msemaji wa Serikali ya Afrika ya Kusini anabainisha kwamba, wakati hii, hali ya Mzee
Mandela ni tete na kwamba, amelazwa mjini Pretoria.