Siku kuu ya Moyo Mtakatifu wa Yesu; waombeeni Mapadre wenu!
Baba Mtakatifu Francisko anawaalika waamini na watu wote wenye mapenzi mema kumshukuru
Mungu kwa zawadi ya maisha na miito ya Kipadre. Anawataka kuwasindikiza Mapadre wao
kwa njia ya sala, wema na ushauri mzuri. Baba Mtakatifu ameyasema hayo wakati alipokuwa
anawapongeza Mapadre wapya kutoka Poland walioshiriki katika Katekesi yake kwa siku
ya jumatano aliyokazia kwa namna ya pekee umuhimu wa utunzaji wa mazingira na hifadhi
kwa binadamu.
Katika Siku kuu ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Baba Mtakatifu anawaalika
Mapadre kumshukuru Mungu kwa zawadi na maisha ya Kipadre. Anawaalika kwa namna ya
pekee kukuza ndani mwao mwanga na nguvu ya Roho Mtakatifu, ili waweze kumtumikia Mungu
na jirani zao kwa ari na moyo mkuu, daima wakichuchumilia utakatifu wa maisha.