2013-06-07 15:23:28

Papa aasa utume wa kidiplomasia si ajira bali ni utumishi


Baba Mtakatifu Fransisko, Alhamisi alizungumza na mapadre wanafunzi katika aasisi ya Elimu ya Kikanisa, ambayo hujishughulisha mafunzo kwa Mapadre walio chaguliwa kuingia katika utume wa ofisi za Kidiplomasia za Kibalozi na katika Sekretarieti ya Jimbo la Takatifu.

Katika hotuba yake, Baba Mtakatifu aliwakumbusha Mapadre wanafunzi kwamba ni lazima wapandikize kwa kina maisha ya kiroho kwa ajii ya kuweza kupata uhuru wa ndani,ambacho ni kigezo muhimu kwa kazi yao ya baadaye. Pia alionya dhidi ya tamaa za kutaka kupanda madaraja , akishutumu kwa mara ingine, kuuchukulia utume huu kama vile ni ajira, akiuita moyo wa namna hiyo kuwa sawa na ukoma.

Papa Francis alitoa maelezo yake kwa kutazama sana mfano wa maisha ya Mwenye Heri Papa Yohane XXIII, akisema ni mfano wa kuigwa na wale wanaotaka kuwa wanadiplomasia.
Papa pia alitoa shukurani za kipekee maalum kwa Masista wote wanaofanyakazi katika Chuo hiki cha Kipapa, kwa huduma yao nzuri na majitoleo na upendo wao, katika kumtumikia Bwana.

MwishoPapa aliomba sala za mapadre kwa ajili yake mwenyewe na aliwakabidhi katika ulinzi wa Mama Bikira Maria na kwa Mtakatifu Anthony Abbate msimamizi wao. Na aliwahakikishia sala na baraka zake, wakati wote wa majiundo yao.








All the contents on this site are copyrighted ©.