Padre Fernando Domingues ateuliwa kuwa Katibu mkuu Shirika la Kipapa la Mtakatifu
Petro
Kardinali Fernando Filoni, Mwenyekiti wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa watu,
amemteua Mheshimiwa Padre Fernando Domingues kuwa katibu mkuu wa Shirika la Kipapa
la Mtakatifu Petro ambalo linajihusisha kikamilifu kwa ajili ya majiundo ya Mapadre
mahalia na kwa sasa linajihusisha pia na majiundo ya Majandokasisi katika nchi za
Kimissionari.
Padre Fernando Domingues mwenye umri wa miaka 54 hadi kuteuliwa
kwake alikuwa ni Gombera wa Chuo Kikuu cha Kipapa cha Urbaniana kuanzia mwaka 2005.