Papa Francis asema kumlilia Mungu wakati wa shida si dhambi
Kumlalamikia Mungu wakati wa mateso si dhambi ila ni sala inayotoka ndani ya Moyo
wa muumini kwa Bwana wake. . Ni tafakari ya Papa Fransisko wakati wa Ibada ya Misa,
Jumatano asubuhi, katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta la Vatican. Ibada iliyohudhuriwa
na baadhi ya wajumbe wa Shirika la Kipapa kwa ajili ya Ibada na Nidhamu katika Sakramenti
, pia walikuwepo wafanyakazi wa Idara ya Maktaba ya Kitume ya Vatican. Papa alisaidiana
na Kardinali Antonio CaƱizares Llovera; Askofu Mkuu Joseph DiNoia,na Monsignor Cesare
Pasini. Homilia ya Papa ililenga zaidi katika ujumbe wa somo la kwanza, maana
ya maisha ya kuteseka ya Tobiti na Sara. Tobit, aliye pofuka licha ya kuwa mtu mwema,
aliyetenda mengi mema na hata kuhatarisha maisha yake. Na Sara, mwanamke aliyeposwa
na wanaume saba , na wote kufariki usiku wa kabla ya harusi. Papa anasema,watu
hao, kila mmoja alimlalamikia Bwana uchungu mkali toka moyoni mwake. Waliomba kwa
Mungu, hata kifo kiwafike, na walijaribu kila njia ya kujiondoa katika matatizo yao.
Walimlalmikia Mungu lakini hawakukufuru. Na hivyo, hili linatuonyesha kwamba, kuomboleza
mbele ya Mungu si dhambi. Papa alieleza na kutoa mfano mwingine wa mama mmoja
aliyekwenda kwa Padre, kumlalamikia Mungu kwa Mateso anayoyapata.Na Padre alimwambia
mwanamke huyo, Mama malalamiko ni sehemu ya sala zako hivyo endelea nayo, Bwana anasikia,
malalamiko yako. Papa aliendelea kutaja mifano mingine mingi mbalimbali ya watu
walioteseka mfano wa Ayubu, aliyesema, na ilaaniwe siku niliyozaliwa, na Yeremia,
pia alimlalamikia Mungu akisema na ilaaniwe siku niliyozaliwa. Siku hiyo mama aliponizaa,
isiwe siku ya Baraka. Papa anasema, kwa ubinadamu wao, waliyalalamikia mateso yao
kwa Bwana, lakiini hawakukufuru.
Baba Mtakatifu pia aliyatazama malalamiko
ya watu wa kale katika mateso, akilinganisha na wakati wetu, kwa mfano watoto wanaoishi
katika mazingira magumu na hatarishi mitaani, wale wenye utapiamlo mkali, wakimbizi
na wagonjwa mahututi n.k. Na alionya dhidi ya kufikiria mateso ya wengine kijuu
juu bila ya kuwa na bidii za kufanya linalo wezekana kuwasidia katika mateso yao.
Alikemea tabia ya kuzungumzia hali ngumu kwa namna za kitaalumbila ya kutazama utu
na heshima yao kama binadamu. Alisema, hata katika kanisa kuna watu wengi katika hali
hii..
Papa amehimiza katika hali hizo , Mkrisu anapaswa kufanya kama Yesu
alivyosema, salini, kwa ajili yao. Sala hizo ni lazima zitoke ndani ya moyo, ni lazima
iwe sababu ya kukosa utulivu wa kiroho kwa ajili ya mateso binafsi, na kwa ajili ya
ndugu zetu walio katika mateso na kifo. Kumwomba Bwana kutoka kina cha moyo na si
kulalama tu kijuujuu. Papa alimalizia kwa kutoa wito kwa waamini wote, kuomba kwa
uaminifu kwa ajili ya wale ambao wanaishi hali ya mateso makubwa kama vile Yesu
juu ya msalabani ,wanalia Baba, Baba, kwa nini umeniacha? Tusali ili maombi yetu
yafike mbinguni na iwe chanzo cha matumaini kwa sisi wote.