2013-06-05 14:57:33

Papa asema unafiki ni ukana Mungu


Papa Fransisko anawaonya Wakristu, kujiweka mbali na lugha ya unafiki kwa kuwa unafiki huweza kuonyesha kama vile yote ni haki, lakini kumbe ni sababu za uongo. Na hivyo Mkristo anapoitanganza Injili, hapaswi kutumia lugha ya kinafiki , lakini kusema ukweli wa Injili na uwazi kama asemavyo mtoto mdogo. Na kwamba “Hakuna ukweli bila ya upendo, maana upendo ni Ukweli”. Ni mafundisho ya Papa Fransisko wakati ya Ibada ya Misa siku ya Jumanne, aliyoiongoza katika katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta la ndani ya Vatican.

Papa baada ya kuzungumzia juu ya ukana Mungu siku ya Jumatatu, Jumanne aliendelea kuitazama lugha ya wanafiki, akiangalisha katika somo la Injili ya siku: lililo lenga katika malipo ya kodi ya Kaisari, na Mafarisayo na Waherodiani, wakimhoji Yesu kwa hila, juu ya uhalali wa kodi hiyo.

Papa Fransisko alibainisha nia na mbinu ya mafarisayo ya kumtega Yesu kwa hila, iliajibu tofauti nayale anayoyahubiri , swali kama ni halali au si halali kulipa kodi kwa Kaisari, tena waliuliza kwa ugha laini, na maneno mazuri, huku wakijionyesha kama ni marafiki, na kumbe ni wanafiki. Ndani mwao, hawana ukweli, ila uongo na unafiki , wakijifunika kwa lugha nzuri ya uongo. Lugha ya kulaghai na kuwajaribu wengine kwa hila, majaribu ya kuwaangusha kiimani kupitia ujanja wa lungha danganyifu na uongo. Wao wana mioyo ya uongo, isiyo kuwa na ukweli.

Papa ameiita lugha hii ya kinafiki kwamba haina tofautina ukani Mungu. Yesu aliwaasa wanafunzi wake wajiepushe na lugha hiyo, bali wausimamie ukweli ambao ni upendo. Unafiki lugha ya ukweli maana ukweli daima hujitenga na uongo. Hakuna ukweli bila upendo . Kama hakuna upendo , hakuna pia ukweli. Na kwamba daima wanafiki wanataka ukweli uliofungamanishwa na maslahi yao kwa mbinu nyingi tofauti tofauti kama ubinafsi, miungu ya unyonyaji a kutaka kunufaika toka kwa wengine, wenye kuwaongoza katika kuwasaliti wengine na wenye kuwaongoza katika madhulumu na unyanyasaji wa uaminifu.

Papa Francis iliendelea, kuzungumuzia lugha hii ya kinafiki kwamba imejaa radha ya kejeli na uongo, kama ilivyokuwa Siku ya Alhamis Kuu, walipomtuhumu Yesu na kumkamana na kumpeleka kwa Pilato , siku ya Ijumaa, Yesu aliutetea ukweli hadi msalabani, bila ya lugha ya kinafiki.
Ndivyo Yesu anavyowataka wafuasi wake wawe. Kusimamia ukweli katika hali zote, kama alivyo mtoto mdogo .
Papa alikamilisha homilia yake kwa kumwomba Bwana, ili kwamba leo hii lugha ya wafuasi wake iwe ni lugha nyepesi , lugha yenye ukweli kama wa mtoto mdogo, ambayo ni lugha ya kimungu na lugha ya ukweli katika upendo.








All the contents on this site are copyrighted ©.