2013-06-04 15:50:50

Papa Fransisko aalikwa kuitembelea Uganda.


Jumatatu katika kuadhimisha siku ya kumbukumbu ya wafia dini wa Uganda , mwaliko ulitolewa kwa Papa Francis kuitembelea Uganda. Mwaliko huo ulitolewa na Askofu Mkuu Paul Bakyenga wa Jimbo Kuu la Mbarara, siku ya Jumatatu , wakati akiongoza Ibada ya Misa kwa nia adhimisho la miaka 125, ya wafiadini wa Uganda.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, maelfu ya waaamini walianza kumininika mjini Mbarara, ili Jumatatu waweze kushiriki katika maadhimisho ya miaka 125 ya Wafia dini wa Uganda. Ibada iliyofanyika katika Madhabahu ya Namugongo,iliyo anza majira ya saa nne za asubuhi Jumatatu, kuenzi na kumsifa Mungu kwa ajili ya ushupavu wawafia dini hao.

Wakatoliki wafia dini wa Uganda waliuawa 1886, kwa amri ya Kabaka Mutesa kwa kuwa walikataa kuikana imani Katoliki. Kwa heshima yao Madhabahu yamejengwa mahali alipouawa Mtakatifu Charles Lwanga kwa kuchomwa moto kwa kuwa alikataa kuukana ukatoliki.
Taarifa zinasema, kwa muda wa siku kadhaa kabla ya adhimisho, mahujaji na waaamini walifuata nyayo za mateso na sulubu walizopitia wafia dini 22 wa Uganda kwa Ibada , tafakari na mafungo binafsi. Na kwamba tukio zima lilipambwa kwa nyimbo na utamaduni mahalia wa kabila la Wanyankole .Na mahujaji bila ya kujali ukali wa jua lililokuwa likiwaka , waliendelea kuimba na kutolea sala, maombi na kumsifu Mungu . Hija hii imetajwa kuwa iliandaliwa vyema na imependeza na kuwa kivutio kwa watu wengi kushiriki.








All the contents on this site are copyrighted ©.