Japan kusaidia kugharimia mchakato wa maendeleo Ukanda wa Sahel
Waziri mkuu wa Japan Shinzo Abe ametangaza kwamba, Serikali yake itagharimia kiasi
cha Euro billioni 770 kwa ajili ya kugharimia shughuli za amani na maendeleo Ukanda
wa Sahel. Waziri Mkuu Abe ameyasema hayo wakati wa kufunga mkutano wa kimataifa wa
maendeleo Barani Afrika uliokuwa unafanyika nchini Japan kwa kuwashirikisha viongozi
kadhaa kutoka nchi za Umoja wa Afrika na Mashirika ya Umoja wa Mataifa.