Imetimia miaka hamsini tangu kutokea kifo cha Papa Yohane XX111
Jumatatu katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, Vatican, Papa Fransisko , alikutana
na kikundi cha mahujaji kutoka Jimbo Katoliki la Bergamo Italia, kikiongozwa na Askofu
Francesco Beschi, ambacho kilifanya hija Vatican, kwa ajili ya maadhimisho ya miaka
50 tangu kutokea kifo cha mmoja wao, Mwenye Heri Papa Yohane XXIII,kwa jina jingine
Angelo RONCALLI .
Katika hotuba yake, Papa Fransisko, alirejesha fikira zake
wakati huo wa miaka 50 iliyopita ambako Mwenye Heri alifariki dunia, akisema kwa
watu wa umri wake Papa Fransisko, bado wanazo kumbukumbu hai za siku hizo za mwisho
wa maisha ya Papa Mwema, ambamo ujumbe wa kifo chake ulienea kwa haraka sana duniani
kote na uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, kuwa mahali patakatifu na wazi kwa
wote usiku na mchana, kutolea maombi yao kwa ajili ya Papa Mwema. Papa Fransisko
amemtaja hayati Papa Yohane XXIII kuwa, alitambuliwa na dunia kuwa ni Papa Mwema,
Mchungaji na baba wa wote, kutokana na sifa zake kuwa ni unyenyekevu na amani,
mambao mawili yaliyojijenga ndani mwake na kuwa mfumo wa tabia yake Askofu Mkuu RONCALLI.
Unyenyekevu na amani ni ahadi yake ya tangu siku alipowekwa wakfu wa Askofu, kama
jarida la Soul toleo la 13-17 Machi 1925 lilivyoeleza. .
Papa Fransisko amesema,
Papa Yohane XX111, alitambuliwa kuwa mtu mwenye uwezo pia wa kuiwasilisha amani katika
asili yake ya utulivu na kirafiki , amani aliyo onyesha kuwa nayo hata kabla ya kuchaguliwa
kuwa Papa, akiitwa Baba Mwema. Fadhila hii ya wema na amani, vilimwenzesha kujenga
urafiki wa nguvu kila mahali na hasa wakati akiwa mwakilishi wa Papa, utume alioufanya
kipindi cha karibia miongo mitatu, akijihusisha kwa karibu na mazingira yanayomzuguka
na pia sehemu zingine za mbali zilizo sahaulika katika ulimwengu Katoliki. Alikuwa
ni mfumaji hodari na fanisi katika ujenzi wa mahusiano na mkuzaji mzuri wa umoja
na shikamano ndani na nje ya jumuiya ya Kanisa. Ndiye aliyeifungua milango ya mazungumzano
kati ya Wakatoliki na Wakristo wa Makanisa mengine, na pia hata kwa wasiokuwa Wakristu,
Wayahudi na Waislamu na waamini wa madhehebu mengine mengi, na watu wote wenye
watu wa mapenzi mema. Papa Fransisko amekiriā Kwa kweli, Papa Yohana XX111, aliipeleka
amani kwa watu wote kwa hekima na busara , juhudi zilizotoa matunda ya kazi ya muda
mrefu na changamoto nyingi binafsi na hivyo kukatika kwa maisha yake, kuliacha mengi
ya kufuatiliwa juu ya maisha yake. Papa Fransisko amemtaja Papa Mwema, kuwa
mfano bora wa imani na fadhila ya kuigwa, si tu na watu wa Bergamo lakini kwa watu
wa vizazi vyote vya Kikristu duniani. Papa alitolea sala ili roho yake iendelee
kuimarisha utafiti wa maisha yake na maandishi yake, lakini juu ya yote, kuiga utakatifu
wake. Na kutoka mbinguni, aweze kuendelea kuliongoza kwa upendo Kanisa la Kristu
ambalo yeye mwanyewe alilipenda katika maisha yake yote. Na pia ili aweze kupata
toka kwa Mungu, zawadi ya miito mingi ya Upadre , miito ya kitawa na maisha ya kimisionari
na pia kwa ajii ya maisha ya familia na uwajibikaji wa walei katika Kanisa na ulimwengu
Ujumla.