Chombo cha kufuatilia maendeleo Tanzania chaanzishwa!
Rais Jakaya Mrisho Kiwete wa Tanzania kwa Mamlaka aliyopewa chini ya kifungu cha 5(51)
cha Sheria ya Majukumu ya Mawaziri The Ministers (Discharge of Ministerial Functions)Act,
sura ya 299 ameanzisha Chombo cha Kusimamia Ufuatiliaji wa utekelezaji wa program
na Miradi ya Maendeleo kwenye Maendeo ya Kimkakati ya Kitaifa (National Key Result
Areas) kinachojulikana kama “President’s Delivery Bureau (PDB)”.
PDB itakuwa
chini ya Ofisi ya Rais, Ikulu na itakuwa na majukumu yafuatayo:-
Kufuatilia
na kutathmini utekelezaji wa Programu na miradi kwenye Maeneo ya kimkakati ya Kitaifa
yanayohitaji matokeo ya haraka.
Kuwezesha ufafanuzi wa kina na program kwenye
maeneo ya Kimkakati ya Kitaifa yanayohitaji matokeo ya haraka.
Kuwezesha na
kufanikisha kuanzisha program na miradi kwenye Maeneo ya Kimkakati ya Kitaifa yanayohitaji
matokeo ya haraka.
Kuwezesha kutambua na kuainisha Maeneo ya Kimkakati ya Kitaifa
yanayohitaji matokeo ya haraka.
Kusaidia kutoa uchambuzi na mapendekezo ya
namna ya kukabiliana na changamoto maalum za utekelezaji.
Kushirikisha umma
kwenye Program na miradi iliyoainishwa kwenye maeneo ya kipaumbele.
Kuandaa
taarifa za utendaji kwa kipindi maalum kwenye Maeneo ya Kimkakati ya Kitaifa na kuziwasilisha
kwenye mamlaka husika.
Kutoa ushauri wa kitaalam wa ndani na kuishauri Serikali
kwenye maeneo ya Kimkakati ya Kitaifa.
Kupanga na kusimamia uendeshaji wa shughuli
za ‘Labs’.
Kuwezesha usimamizi wa mikataba ya utendaji kwa Mawaziri wanaouhusika
na program na miradi ya kipaumbele iliyo chini ya Wizara zao.
Kuwezesha na
kusimamia uandaaji wa viashiria vikuu vya utendaji (Key Performance Indicators) vya
kitaifa na kiwizara kwenye program na miradi ya kipaumbele.
Kufanya uhakiki
wa utendaji wa Mawaziri kwenye Maeneo ya Kimkakati ya kitaifa yanayohitaji matokeo
ya haraka.
Kuwezesha uhakiki wa utendaji wa PDB.
Aidha, taarifa
ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Y. Sefue imesema kwamba, Mheshimiwa Rais pia
amemteua Ndugu OMARI ISSA kuwa Mtendaji Mkuu wa kwanza wa PDB kuanzia tarehe 01 Juni,
2013. Ndugu Omari Issa ni Mtanzania mwenye uzoefu mkubwa ndani na nje ya nchi, barani
Afrika na duniani, kwenye sekta ya umma na sekta binafsi, na kwenye ulimwengu wa biashahra
na utendaji wa makampuni makubwa ya kimataifa.
Rais anaamini kuwa uzoefu
huo na utamaduni huo wa utendaji katika sekta binafsi katika ngazi hiyo utakuwa mchango
mkubwa na muhimu katika siku za mwanzo za President’s Delivery Bureau na ubadilishaji
wa utamaduni wa utendaji Serikalini kwenye maeneo ya kipaumbele. Ndugu OMARI ISSA
alikuwa Mtendaji Mkuu wa kwanza wa “Investment Climate Facility for Africa”.