Kanisa linapata chimbuko lake kutokana na upendo wa Kristo Msalabani!
Baba Mtakatifu Francisko anawaambia watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, Kanisa
linapata chimbuko lake kutokana na sadaka ya upendo wa Kristo Msalabani, pale alipotobolewa
ubavu, humo ikatoka damu na maji, alama ya Sakramenti za Kanisa. Kanisa ni familia
ambamo mtu anapenda na kupendwa.