2013-05-25 15:52:36

Usafirishaji wa watu kinyume na haki, ni fedheha kubwa isiyoweza kuvumiliwa.


Baba Mtakatifu Fransisko, amelaani vikali uwepo wa mipango ya kusafirisha watu kinyume na haki za binadamu. Kemeo hilo alilitoa wakati akikutana na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza kwa ajili ya Huduma za Kichungaji kwa wahamiaji na watu wasiokuwa na makazi maalum, ambao wapo Roma kwa ajili ya kuhudhuria vikao vya Mkutano wa Baraza wa Mwaka vilivyoanza siku ya Jumatano. Mada kuu ya Mkutano huo ni “Watu waliolazimishwa kuhama makazi yao”. Baraza linatazama kwa makini kwa jinisi gani Kanisa linaweza kutoa msaada wa kufaa kwa watu hao.
Katika hotuba yake, Papa ameonyesha kujali mwelekeo wa kukua kwa wimbi la watu kulazimishwa kuhama makazi yao kwa namna mbalimbali na hasa mipango ya kurubuni watu kwenda maeneo ya mbali na makazi yao kwa muono kwamba wanakopelekwa watapata ajira na kumbe sivyo. Papa ameiita mipango hiyo haramu ya kusafirisha watu kwa nia mbovu, kuwa ni fedheha kubwa inayo dharirisha ubinadamu wa mtu.
Kwa ajili yaowatu hawa wanaodharirishwa, Papa ametoa wito kwa mataifa kuchukua hatua za kulinda utu wa watu hao kama jambo la kidharura.
Alisistiza usafirishaji wa watu ni ujinga na aibu kwa jamii yetu inayojiita imestraabika. Wanyonyaji na wabia wao wote na katika ngazi zote za biashara hii, wanapaswa kuchunguza kwa makini dhamiri zao wenyewe na mbele ya Mungu. "
Papa amesisitiza, Kanisa kwa mara nyingine, linarudia kutoa ombi lake kwa nguvu, kwamba ni lazima kutunza na kulinda hadhi na utu wa binadamu. Na hiyo ina maana ya kuheshima haki za msingi kwa kila binadamu. Ni jambo la aibu kusikika kuna watu wanaodiriki kuuza wenzao kama vileni bidhaa, katika dunia ambamo kuna majadiliano mengi ya haki. Inafedhehesha kusikia wtu wanapuuza haki na maazimio ya Umoja wa Mataifa na kufinyanga haki na utu wa mtu, katika dunia ambamo watu wanazungumza kuhusu haki.
Papa Fransisko analaani utafutaji wa fedha wa namna hiyo kuwa ni balaa na fedh ainayopatikana ni chafu . Alieleza na kuonyesha kujali kwamba sasa tunaishi katika dunia ya kujali fedha. Tunaishi katika ulimwengu, na katika utamaduni wa ufalme wa fedha.
Ni lazima kuukataa ufalme huo wa tamaa za kujilimbikia fedha wenye kufisha heshima ya Utu wa mtu. Ufalme unaopokonya mastahili hasa ya watu wanyonge na maskini , kuwadharirisha na kuwapuuza.
Papa Fransisko ametoa ombi kwa watawala na wabunge wa kila jumuiya kitaifa na kimataifa, kulitazama jambo hili kwa makini na kukomesha madhulumu yote.
Papa, umezitazama hali halisi ya watu waliolazimishwa wakiyakimbia makazi yao akisisitiza, mipango madhubuti na mbinu mpya ziandaliwe, ili kulinda heshima ya wanaokumbana na matatizo hayo na maisha yao yaboreshwe na kupata msaada katika kukabiliana na changamoto zinazoibuka kutokana njia za kisasa za ukandamizaji mateso, na utumwa.
Papa anawaombea wote walioingizwa katika madhulumu haya makali , ili waweze kupata nguvu za kurejesha maisha yao kawaida, kwa uvumilivu, saburi , furaha na upendo. Na kwamba sote tunapaswa kulisha tumaini la watu hawa.








All the contents on this site are copyrighted ©.