2013-05-25 16:05:47

Papa Fransisko: Kuteseka na hali ngumu kwa uvumilivu na kushinda ugandamizwaji kwa upendo.



Mkristu anapaswa kustahimili, kuvumilia mateso, na kushinda ukandamizwaji wa nje na ndani, kwa upendo , ni msisitizo uliotolewa na Papa Fransisko wakati akiongoza Ibada ya Misa katika Kanisa la Mtakatifu Marta mapema asubuhi siku ya Ijumaa, ambayo ilikuwa ni Siku Kuu ya Mama Maria, Msaada wa Wakristo.

Katika hotuba yake, Papa Fransisko , aliomba neema mbili ambazo ni kustahimili kwa uvumilivu na kupata ushindi kwa njia ya upendo. Alitaja hizi ni neema mbili halisi kwa Mkristu. Papa alionyesha kutambua kwamba, uvumilivu katika mateso, si jambo jepesi katika hali zote iwe mateso ya kiroho au kimwili au kutokana na matatizo mengine ya nje ya kijamii, bado ni mateso yanayoumiza roho ya mtu. Lakini katika kuteseka Papa anasema si tu kama jambo jepesi la kuyavumilia mateso, lakini ni wakati wa kuyabeba mateso kwa nguvu zaidi ili kwamba matatizo hayo, yasituangushwe chini.

Ni kuendelea kuwa imara na tena kwa ushupavu zaidi. Huo ndiyo uadilifu wa Kikristo. Papa alieleza na kumrejea Mtakatifu Paulo, anaongea mara kadhaa juu ya kupokea na kuyavumilia mateso, kwa ushupavu zaidi, kukataa kushindwa na matatizo. Na hili linapata maana kwamba, kwa Mkristo, mateso ni kigezo cha kuiimarisha zaidi imani yake.
Ingawa si jambo jepesi, na hasa kutokana na vishawishi vya mambo mengine yanayolenga kudhoofisha imani, Mkristu anapaswa kuvikataa vishawishi hivyo na kuyavumilia mateso kama silaha yake ya kumuirisha zaidi, kwa muono kwamba, mateso ni neema kuvumilia. Na hivyo katika matatizo ni lazima kuiomba neema hii .
Papa aliiigeukia neema ya ushindi kwa upendo, akisema, kuna njia nyingi za kupata ushindi lakini kwa neema ya upendo tunayoimba, nayo pia si rahisi, hasa pale tunapokuwa na maadui nje wanao tupata mateso makubwa , inakuwa ni mtihani mgumu kuupata ushindi kwa njia ya upendo. Mara nyingi kishawishi cha kutaka kulipiza kisasi huonekana kwa nguvu zaidi, kama ndiyo jibu sahihi la kuzia mashambulizi dhidi ya adui. Lakini Yesu alitufundisha kuwa wanyenyekevu na pole, kwamba upole ni ushindi, kama Mtume Yohana anatuambia katika barua yake ya kwanza: Upendo ni ushindi wetu, na imani yetu'. Imani yetu ni kwamba , Yesu, alitufundisha upendo na alitufundisha kumpenda kila mtu. Na kwamba, sisi tunakuwa na upendo wakati tunapowaombea adui zetu, na kuwapenda.

Ingawa kuwaombea maadui zetu wanaotufanya tuteseke pia si jambo jepesi , lakini Mkristu hupata nguvu za kufanya hivyo kwa utambuzi kwamba , ushindi wake unaweza kupotea, pale anaposhindwa kusamehe maadui na kama hawezi kuomba kwa ajili yao. Na hivyo ndivyo ilivyo kwa Wakristo wanaye shindwa kuomba neema hii ya upendo, humezwa na huzuni na kukata tamaa, kwa sababu hana tena neema ya kustahilimili, uvumilivu na ushindi kwa upendo":

Papa alikamilisha homilia yake akiomba msaaada wa Mama Maria, Msaada wa Wakristu , ili Bwana awajalie wafuasi wake Neema ya neema ya kustahimili , uvumilivu na kushinda kwa upendo. Na kwmaba kuna wengi walioichukua njia hii nzuri , ambao hawana mengi ya kueleza ili miyo yao imejazwa na upendo. Wnajua namna ya kumsamehe adui na wanajua jinsi ya kuwaombea Maadui . Na hivyo ndivyo Wakristo wanayotakiwa kufanya.

Ibada hii ya Misa ilihudhuriwa na wafanyakazi katika Baraza la Kipapa kwa ajili ya Mawasiliano Jamii, akiwepo pia Rasi wa Baraza hilo, Askofu Mkuu Claudio Maria Celli. Siku hiyo pia Mama Kanisa alikuwa akitolea maombi yake kwa ajili ya Kanisa nchini China. Katibu Mkuu wa Shirika kwa ajili ya Uinjilishaji wa Watu , na kikundi cha Mapadre , watawa na Waseminaristi na walei kutoka China pia walihudhuria Ibada hiyo.








All the contents on this site are copyrighted ©.