Wapenda haki na amani wasikitishwa na vitendo vya vurugu nchini Tanzania!
Askofu mkuu Protase Rugambwa, Katibu mwambata na Rais wa Mashirika ya Kipapa ya Kazi
za Kimissionari katika mahojiano maalum na Radio Vatican anasema, matukio ya uvunjifu
wa misingi ya haki, amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa nchini Tanzania ni changamoto
na tatizo kubwa linalopaswa kushughulikiwa kwa umakini mkubwa.
Watanzania
wote kila mtu kaadiri ya uwezo wake, wakae pamoja na kuanza mchakato utakaolisaidia
taifa kurudi katika hali yake ya zamani, iliyoitambulisha kuwa ni kisiwa cha amani.
Askofu mkuu Rugambwa anapenda kuchukua nafasi hii kutuma salam zake za rambi rambi
kwa wote waliofikwa na majanga ya madhulumu ya kidini pamoja na ghasia zinazoendelea
kufuka moshi. Anatoa pole pia kwa wale wote walioathirika kwa namna moja au nyingine.
Anasema, amani ni jambo la msingi kwa ustawi na maendeleo ya watu.