2013-05-23 14:49:05

Ubinafsi unaendelea kusababisha maafa Mtwara!


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi wa Tanzania Dk. Emmanuel Nchimbi alionya kuwa tabia na inayoanza kujengeka ya kila eneo kutaka inufaike peke yake kutokana ralimalia ya taifa iliyopo kwenye eneo husika italigawa taifa. Dk. Nchimbi amesema kuna baadhi ya taasisi za kiraia na vyama vya siasa kutokana na maslahi binafsi yasiyo na upeo mpana vinaweza kudhani kuunga mkono madai ya namna hiyo vinaweza kukubalika na jamii.

Alisema watu kama hao wataipasua nchi na kusababisha vifo vya maelfu na majeruhi huku akimtaka kila kiongozi na mwananchi atambue anayo dhamana ya kuendeleza haki, amani na kuchangia maendeleo. Amesema wapo wasaliti wa taifa la Tanzania ambao wanajua maendeleo makubwa yanayoweza kupatikana Mkoani Mtwara na Tanzania kwa ujumla kutokana na gesi hivyo, wanatumia vibaya ufahamu wao mdogo kuhusu gesi na kuchochea upinzani dhidi ya mradi huu unaotarajiwa kuwakomboa Wanamtwara na Watanzania kwa ujumla.

Akizungumzia kuhusu vurugu hizo, Waziri Nchimbi amesema jumla ya watu 91 wamekamatwa kwa makosa ya kufanya mikusanyiko isiyo halali na uharibifu wa miundombinu. Amesema hata hivyo vurugu zimedhibitiwa huku polisi wakiendeleza oparesheni ya kuhakikisha hali ya usalama inarejea huku akiwapongeza kwa kazi waliyofanya pamoja na uchache wao.

Katika hatua nyingine alisema askari wanne kati ya 32 wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kutoka Nachingwe waliokuwa wakienda mjini humo kuongeza nguvu za kudhibiti vurugu hizo walikufa baada ya gari la kupata ajali huku 20 wakijeruhiwa. Waziri wa Mambo ya Nani ya Nchi amesema kuwa hadi sasa mtu mmoja aliyefahamika kama Karim Shaibu katika vurugu hizo wakati Askari Polisi wawili walijeruhiwa kwa bomu la kishindo.

Akizungumzia kuhusu uharibifu uliotokea amesema ofisi ya Mbunge wa Mtwara Mjini, Hasnain Murji (CCM) iliyopo Mikindani imeharibiwa vibaya na kuharibiwa vitu vilivyokuwemo wakati nyumba za askari wanne zimevunjwa na kubwa vitu mbalimbali.

Ameongeza kuwa ofisi ya Mahakama ya Mwanzo, ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Chikongola, nyumba ya mwandishi wa habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Kassimu Mikongoro zimechomwa moto. Pia nyumba ya ofisa Mtendaji Kata ya Magomeni imechomwa moto lakini Nchimbi amesema bado thamani halisi ya mali zote zilizoungua na kuharibiwa bado haijapatikana.








All the contents on this site are copyrighted ©.