2013-05-23 15:08:06

Ripoti ya mwaka ya Mamlaka ya Usimamizi wa fedha za Vatican


Jumatano, Ofisi ya habari ya Vatican, ilikuwa mwenyeji wa Mkutano kwa ajili ya uzinduzi wa Ripoti ya Mwaka 2012 ya Mamlaka ya Fedha (AIF). Mkurugenzi wa Mamlaka hayo , Rene Brülhart, alitaja ushirikiano wa ofisi mbalimbali za Vatican katika kukabiliana na matumizi mabaya ya mfumo wa fedha wa Vatican.
AIF ni mamlaka husika ya Jimbo Takatifu na Nchi ya Vatican, kwa ajili ya usimamizi na udhibiti wa fedha zinazopita ktatika mfumo wa fedha wa Vatican, zisitumike kufadhili ugaidi. AIF ilianzishwa mwaka 2010 na kuanza kazi zake rasmi Aprili ya 2011.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ofisi ya Habari ya Fedha katika mamlaka ya AIF, ya Jimbo Takatifu na nchi ya Vatican kuchapisha na kuwasilishwa taarifa yake ya mwaka hadharani. Ripoti hiyo ni mapitio juu ya shughuli na takwimu za AIF, kwa mwaka mzima 2012.
Ripoti inabaini, katika kipindi hiki cha mwaka 2012 ,AIF, kumetolewa tuhuma sita, katika huduma za kuhamisha na kuingiza fedha katika mfumo wa fedha wa Vatican ambapo mwaka juzi, ilikuwa ni kesi moja tu iliyotolewa. Kati ya kesi hizo sita, mbili ziliwasilishwa katika Kitengo cha sheria cha Vatican kwa uchunguzi zaidi. Na kwamba takwimu na mwelekeo tangu mwanzo wa 2012 unatia moyo na kuonyesha kwamba , mfumo wa fedha unaendelea kuboreshwa.
Rene Brülhart, Mkurugenzi wa AIF, aliendelea kuuambia mkutano kwamba, mwaka 2012, AIF pia ilianzisha mfumo wa kuchunguza utaratibu katika uchambuzi wa uhamishaji wa Fedha kwa mujibu wa vyombo vya kisheria, katika kukabiliana kikamilifu na matumizi mabaya ya uwezo wa mfumo wa fedha wa Jimbo Takatifu na Vatican. Juhudi hizi walizifanya kwa kushirikiana kwa ukaribu zaidi na Sekretarieti ya Nchi, Mfumo wa Ulinzi wa Vatican (Gendarmeria), na watetezi wa Sheria na taasisi chini ya usimamizi wa AIF, ili kuboresha ufahamu na usalama, na kuhakikisha uratibu wa ndani ya ushirikiano katika masuala yote ya uingizaji na hamishaji wa fedha kutoka taasisi za fedha za Vatican.
Na zaidi kipengele muhimu katika ripoti hiyo ni mafanikio yaliyopatikana katika ushirikiano wa kimataifa, unaoonyesha wazi uwajibikaji wa Jimbo la Papa katika kuw Mbia aminifu kimataifa, katika lengo la kukabiliana na uwepo wa fedha chafu. Mwaka 2012, kulitiwa saini hati ya Mkataba wa Makubaliano na Mamlaka husika, nchini Ubelgiji na Hispania. Mkataba huo, unaendelea kuwa sera ya utendaji kwa mwaka 2013, ili kuendeleza uimarishaji wa ushirikiano wa kimataifa, katika utiaji wa sahihi katika mikataba kadhaa ya Makubaliano, ushirikiano na Ubia na nchi nyingine husika na mamlaka.
Katika Ripoti hii ya mwaka 2012, Mkurugenzi Rene Brülhart, anasema mtazamo kwa ajili ya 2013 inaendelea kukaza uimarishaji zaidi wa mfumo wa fedha zinazoingia na kutoka AML / CFT, ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Mapendekezo Moneyval kupitia sheria mpya zinazofaa au kufanyiwa marekebisho na mwendelezo wa ufahamu, kwa ajili ya kuimarisha mchakato fedha katika mamlaka zote husika na taasisi.









All the contents on this site are copyrighted ©.