Papa Francisko kutembelea mji wa Assisi hapo tarehe 4 Oktoba 2013
Baba Mtakatifu Francisko amekubali ombi lililotolewa na Askofu Domenico Sorrentino
wa Jimbo la Assisi-Nocera Umbra-Guardo Tadino, nchini Italia la kutembelea Assisi
hapo tarehe 4 Oktoba 2013. Baba Mtakatifu Francisko anasema kwamba, Mji wa Assisi
una umaarufu wake. Anawatakia maandalizi mema kwa ajili ya hija hii ya kichungaji
na anawaomba ili waendelee kumwombea katika maisha na utume wake kama Khalifa wa Mtakatifu
Petro.