2013-05-23 15:27:22

Ijumaa , tuwakumbuke Wakristu wa China katika sala- wito wa Papa


Papa Fransisko ametoa ombi kwa Wakristo duniani kote, Ijumaa ya wiki hii, kutolea sala kwa ajili ya Wakristu nchini China.
Akizungumza mwishoni mwa Katekesi yake kwa mahujaji na wageni waliofika kumsikiliza katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro siku ya Jumatano, Baba Mtakatifu aliutumia muda huo, kutoa ombi lake la kuwataka wakristu duniani kote Ijumaa, Mei 24 2013, waungane katika sala kuwaombea Wakristu wa China.
Tarehe hii 24 Me1, iliwekwa wakfu kwa ajili ya kumbukumbu ya kiliturujia ya Bikira Maria, Msaada wa Wakristo, anayeheshimiwa kwa msisimko mkubwa wa ibada katika Madhabahu ya Sheshani Shanghai, kuwa siku ya kuuungana kiroho kwa ajili ya kuwaombea Wakristu wote wa China.
Alisema, "Naomba Wakatoliki wote duniani kujiunga katika sala pamoja na ndugu na dada zetu wa China, kuomba kwa Mungu, neema ya kutangaza kwa unyenyekevu furaha ya Kristu, aliyekufa na kufufuka, na pia katika kuwa aminifu kwa Kanisa lake na Khalifa wa Mtume Petro, na kuyaishi maisha ya kila siku katika huduma ya taifa lao na kwa wananchi wenzao, kwa njia ambayo ni thabiti katika imani wanayo ikiri.

Papa alitoa ombi lake huku akiongeza kwamba , kwa maneno yetu wenyewe machache ya sala, kwa Mama wa Sheshani, pamoja nanyi, alipenda kutolea sala kwa Mama Bikira Maria: "Mama yetu wa Sheshani, awadumishe waamini wote wa Kanisa nchini China, ambao,licha ya kukabiliwa na majaribumakali kila siku , bado wanaendelea kuamini, kwa matumaini na upendo. Kamwe na wasipatwe na woga na hofu ya kumtangaza Yesu ulimwenguni , na dunia kote.

Papa alisali ili Mama Maria, Bikira mwaminifu, , msaada Wakatoliki Kichina, awe msaada wa kutimiza wajibu wao , licha kwamba si rahisi, lakini wa thamani sana katika macho ya Bwana, katika kuulisha mapenzi na ushiriki wa Kanisa nchini China, kwenye umoja wa hija nzima ya kanisa la Ulimwengu. .


Pia ilikumbusha Mei 2008, Papa-mstaafu, Benedict XVI, alitoa wito kwamba, katika adhimisho la Siku Kuu ya Mama yetu, Msaada wa Wakristo , Siku inayoheshimiwa sana katika Madhabahu ya Sheshani, karibu na Shanghai Mei 24 ya kila mwaka, iwe ni Siku ya Dunia ya kutolea sala maalum kwa ajili ya taifa la China.








All the contents on this site are copyrighted ©.