2013-05-22 15:34:20

Ujumbe wa Papa kwa wahanga wa Kibunga- Oklahoma


Baba Mtakatifu Francis, Jumanne mara baada ya kupata taarifa za kimbunga kikali kilichopita katika mji wa Oklahama Marekani, alipeleka salaam zake za rambirambi kwa waathirika wote na uongozi mahalia kupitia Mjumbe wake Askofu Mkuu Paulo Coakley, Askofu Mkuu wa jiji la Oklahoma.
Katika ujumbe huo, Papa ametaja mshikamano wake wa karibu na wote, kupitia njia ya sala na maombi kwa Bwana mwenye huruma na tumaini la maisha. Na ameonyesha kujali hasara ya kutisha ya maisha yaliyokatizwa na pia kazi kubwa inayowakabili sasa, ya kuujenga upya mji huo na vitongoji vyake.
Na amewaombea wote walio fariki katika janga hili, mapumziko katika amani ya Bwana wa milele, nao wafiwa na walio katika mateso wapate kuwa na faraja za Kristu Mfufuka, licha ya mateso wanayopata sasa, na hasa kwa kukosa makazi au majeruhi.
Kwa namna ya pekee, ametolea sala kwa Mungu mwenye huruma nyingi awafariji hasa vijana na watoto katika wakati huu mgumu wa maombolezo na familia zao.
Pia amewaombea viongozi mahalia na viongozi wa kidini na kwao wote wanaohusika na jitihada za kutoa misaada, wapate zawadi ya Kristu, Bwana wa uweza , nguvu, faraja, na uvumilivu na matumaini mapya mema.


Baba Mtakatifu Francis, Jumanne mara baada ya kupata taarifa za kimbunga kikali kilichopita katika mji wa Oklahama Marekani, alipeleka salaam zake za rambirambi kwa waathirika wote na uongozi mahalia kupitia Mjumbe wake Askofu Mkuu PAULO S. Coakley, Askofu Mkuu wa jiji la Oklahoma.
Katika ujumbe huo, Papa ametaja mshikamano na ukaribu wake kwa wote kupitianjia ya sala namaombi kwa Bwana mwenye huruma na tumaini la maisha. Na ameonyesha kujali hasara ya kutisha ya maisha yaliyokatizwa na pia kazi kubwa inayowakabili sasa, ya kuujenga upya mji huo na vitongoji vyake. Na amewaombea wote walio fariki katika janga hili, mapumziko katika amani ya bwana wa milele, nao wafiwa na walio katika mateso wapate kuwa na faraja za Kristu Mfufuka, licha ya mateso wanayopata sasa, na hasa kwa kukosa makazi au majeruhi.
Kwa namna ya pekee, ametolea sala kwa Mungu mwenye huruma nyingi awafariji hasa vijana na watoto katika wakati huu mgumu wa maombolezo na familia zao.
Pia amewaombea viongozi mahalia na viongozi wa kidini na kwao wote wanaohusika na jitihada za kutoa misaada, wapate zawadi ya Kristu, Bwana wa uweza , nguvu, faraja, na uvumilivu na matumaini mapya mema.








All the contents on this site are copyrighted ©.