2013-05-22 15:31:46

Papa atembelea nyumba ya inayohudumia wahitaji..


Jumanne pia Baba Mtakatifu Fransisko, alitembelea nyumba inayotoa msaada wa kihali kwa maskini inayoitwa "Casa Dono di Maria, inayoendeshwa na Shirika la Upendo la Mama Tereza wa Calcutta.
Papa Fransisko alifanya ziara katika nyumba hii, ililyoko katika kuta za Vatican, kwa nia ya kushiriki adhimisho la miaka 25, tangu kufunguliwa kwake.
Katika hotuba yake , Papa aliiwashukuru kwa dhati, watawa wanaohudumia nyumba hiyo, kwa kujali idadi kubwa ya watu wahitaji, wanaowalisha na kuwanyweshana kutibiwa majeraha na hasa majeraha ya kiroho. Papa aliitaja miaka hii 25 kwamba yote imekuwa ni miaka ya msamaria mwema , anaye mwinamia mhitaji na kumpa msaada , na ndivyo wao pia wanavyokuwa wasamaria wema.
Nyumba hii , iliyoko ndani ya jiji la Vatican karibu na jengo la Ofisi ya Shirika kwa ajili ya Imani Sadikifu, hulisha wastani wa watu maskini 60 kila siku na hutoa nafasi ya malazi kwa wanawake 25. Jengo hili lilizinduliwa na Mwenye Heri Yohane Paulo 11 , kama matokeo ya Mwenye Heri Yohane Paulo 11 kukutana na Mwenyeheri Tereza wa Calcutta.
Papa Fransisko akiwa mahali hapo , alisema jengo hili linapaswa kukumbusha jumuiya ya Wakristu , na kwa jiji lote na wakazi wote wa Roma, kujenga familia thabiti kwa ajili ya kwuapokea wahitaji, ni kuwa na nyumba iliyo tayari kupokea wageni na kuhudumia na kujenga udugu zaidi.
Pia Papa alizumgumzia umuhimu wa mtu kujitolea sadaka kwa uhuru kamili na kuwa tayari kuhudumia mwingine, majitoleo ya kama zawadi kwa wengine, kuwa zawadi huru ya ukarimu na mshikamano. Papa kwa uyenyekevu, aliwapa Baraka zake za Kitume akiwamobea ili Mwenyezi Mungu , awape nguvu za kuendelea na utume huo, ishara wazi ya huruma ya Yesu katika dunia ya leo.








All the contents on this site are copyrighted ©.