Umoja wa Wakristu ni muhimu hata katiak ushirikiano wa kibara
Mchakato wa Wakristu kuungana kiekumene ni muhimu kuchukuliwa kuwa ni mchango mkubwa
katika kudumisha hali halisi za baadaye za siasa ya ubinadamu hasa katika dunia ya
Magharibi. Na hivyo ushindi mpya wa umoja wa makanisa ya Kikristo, unakuwa ni msukumo
mpya katika utendaji wa pamoja wa muungano wa Ulaya hasa katika kupambana na changamoto
zilizpo kama mgogoro wa uchumi. Haya ni maoni ya Kadrinali Kurt Koch, Rais wa
Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza Umoja wa Kikristo, alipo zungumza Ijumaa iliyopita,
wakati wa kukamilisha Mjadala juu ya Pentecoste katika mtazamo wa ushirikiano kati
ya Ulaya na Marekani, majadiliano yaliyofanyika katika Kanisa Schloss Seggau, Austria.
Alisema, katika hali halisi msingi za matatizo ya kiroho barani Ulaya, miongoni
mwa mambo mengine, ni ukana Mungu na ubinafishaji utendaji wa kidini, ambavyo leo
hii vinavyonekana kutaka kuwa tabia ya Ulaya na hivyo kuleta mshuko wa maendeleo
katika ubinadamu, na matokeo yake yasionekana waziwazi lakini yanatisha, kama ilivyokuwa
katika nchi za Magharibi katika karne ya kumi na sita ambamo kulifanyika vita vya
umwagaji damu kwa ajili ya kuttea dini. Kardinali alieleza na kuelekeza mawazo
katika mapambano kati ya Wakatoliki na Waprotestanti,ya karne ya kumi na sita ,
akisema zaidi ya yote , ilikuwa ni ubinafsi wa kimadhehebu,uliosukuma nje umoja
wa Wakristu na amani kijamii. Kardinali Kurt , anaendelea kueleza kwamba Makanisa
haya yote yalifanya makosa makubwa katika muono wa kidini na jamii kwa ujumla. Alieleza
na kurejea maelezo ya mwana teolojia Makatoliki wa Ujeruman, Johann Baptist Metz,aliyesema,
machafuko na utengano huo, ulibinafisisha Ukristo, na kuingiza dini nyenyewe katiak
utengano na machafuko na hivyo ilikuwa ni kuubinya uhuru wa uogofu na utendaji wa
Mkristu katika maisha ya kijamii.
Kwa mujibu wa Kardinali Kurt, Rais wa Baraza
la Kipapa, harakati za kiekumeni, Vikundi vya Kiekumene , vinatakiwa kutenda kinyume
na kila changamoto inayotaka kudhoofisha umoja a Wakristu aliyotamani Yesu mwenyewe.
Pia Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatikani, inaona haja ya kurejesha umoja wa Wakristo
kama moja ya kazi yake kuu. Lakini hili linawezekana tu iwapo Makanisa yataweza kufanya
toba kusameheana na kuridhiana, na kufanya kazi katika hali ya kuaminika kwa ajili
ya uendelezaji wa marekebisho kwa ajili ya ujenzi mpya wa umoja na amani hata kijamii.
Na hii inapaswa kufanywa kupitia maisha ya kushirikishana kwa ajili ya umoja
wa watu", kama ilivyo tajwa katika Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, katika ulimwengu
huu wa watu waliojaw ana roho ya kusambaratika, w chuki na utafutaji wa maslahi
ya kutatanisha kw amanufaa binafisi. Wakati wa kuhitimisha Mkutano, Kardinali
Kurt, alizungumzia uwiano kati ya Ulaya na ekumeni. Na washiriki wote walionekana
kupendelea Uekumene kama neema ya barala Ulaya. Lakini Kardinali aliasa juu ya ukosefu
wa utambuzi, katika utendaji kwamba, neema si rahisi kuwepo iwapo maisha ya kijamii
hayashuhudii umoja na mshikamano wa kiekumene.
Ni kweli kuna mawazo mengi juu
ya umoja ndani ya Makanisa. Lakini, Rais wa Baraza la Kipapa kwa ajili ya Kukuza
Umoja wa Kikristo aliongeza , sera ya Ulaya ni lazima kuwa zaidi ya katoliki kwa
maana ya kuwa na mabadiliko ya wote, na kushukuru kwa ukweli kwamba Papa Francesco,
ametoka Amerika ya Kusini , na hivyo hii inazidi kudhihirisha kwamba Kanisa si la
Ulaya peke yake, lakini kitovu cha dunia kwa ajili ya Wakaristu wote iwe Amerika
ya Kusini, Afrika, Asia Marekani n.k.