Papa anaomboleza kwa wale waliokumbwa na tufani Oklahoma
Baba Mtakatifu Francisko anawaalika watumiaji wa mitandao ya kijamii kuungana pamoja
naye kwa ajili ya kuwaombea watu waliofikwa na maafa huko Oklahoma, nchini Marekani,
baada ya kukumbwa na tufani. Kwa namna ya pekee anaungana na wale ambao wamewapoteza
watoto wao katika tufani hii.