Roho Mtakatifu ni kielelezo cha utulivu, amani na ujasiri!
Katika Maadhimisho ya Sherehe ya Pentekoste, Baba Mtakatifu Francisko amewaambia watumiaji
wa mitandao ya kijamii kwamba, Roho Mtakatifu anageuza na kuwaletea waamini mabadiliko
ya ndani katika maisha yao; Roho Mtakatifu anajenga na kuimarisha utulivu na umoja;
anawakirimia ujasiri na furaha ya utume!