2013-05-20 16:30:19

Imani katika sala, unyenyekevu, na moyo wa ushujaa hutenda miujiza


Sala ujasiri nyenyekevu na uthabiti, hufanikisha miujiza: Papa alieleza hili, mapema Jumatatu wakati akiongoza Ibada ya Misa, katika Kanisa dogo la Mtakatifu Marta la mjini Vatican. Ibada iliyohudhuriwa na baadhi ya wafanyakazi wa Radio Vatican, wakiwa wameandamana na Mkurugenzi wao Padre Federico Lombardi.
Homilia ya Papa kwa wafanyakazi hao, ilirejea Liturujia ya Neno la siku, kifungu cha Injili ambamo wafuasi wa Yesu walishindwa kumponya kijana mdogo mgonjwa, na Yesu aliwajibu kwamba wameshindwa kumponya kijana huyo kwa sababu wana imani haba. Baba wa Kijana huyo kwa imani thabiti, aliomba msaada kwa Yesu. Na Yesu anawaambia kila kitu kinawezekana kwa anayeamini.
Papa Francesco alieleza, mara nyingi wapo wanaopenda kuwa wafuasi wa Yesu, lakini hawapendi kuhatarisha mengine wanaoyoyaamini na hivyo imani yao kwa Kristu inakuwa ni imani nusunusu, hawana imani nae kikamilifu. Papa alieleza na kuhoji kwa nini hali hi ya kutosadiki kikamilifui? Na alitoa jibu kwamba, wao wana amini kwamba, ni moyo wenyewe usiotaka kujifunua wazi, moyo unabaki umefungwa , lakini katika ukweli wake moyo huo unaotamani kuwa na imani thabiti.

Hivyo basi, binadamu anaushinikiza moyo kutojifunua na wala kujiweka chini ya maongozi ya Yesu, kama ilivyokuwa wakati ule, wanafunzi wa Yesu walimwuliza kwa nini, hawakuweza kumponya kijana, na Bwana aliwajibu kwamba aina mapepo yaliyomshambulia kijana huyo, hayawezi kutolewa nje na jambo lolote , isipokuwa kwa sala tu.
Papa alieleza na kusema, ingawa tunamtolea sala Bwana,ndani mwetu tuna kigugumizi cha imani. Hatuna imani thabiti na yule tunayemtolea maombi yetu lakini twayatolea maombi hayo kama majaribio au mazoea ya kusali. Ili Bwana aweze kuyaitikia maombi yetu, twapaswa kusadiki kwamba kile tunachomwomba Bwana atakifanikisha. Na hii ni kuwa na imani thabiti katika nguvu ya sala, ni kusadiki kw unyenyekevu kwamba, Yesu ni nguvu na anaweza kufanya muujiza.
Kuomba muujiza wa uponyaji , au kuomba mabadiliko katika mahusiano ni lazima kuambatane na sala thabiti inayotuhusisha sisi sote. Papa Francisko alieeleza na kutolea mfano wa tukio hilo lilitokea huko Argentina, ambako : mtoto wa miaka 7 aliugua na madaktari kutoa masaa machache ya maisha. Baba yake, fundi umeme, mtu wa imani, akiwa kama amepagawa na habari hii ya maisha ya mtoto wake kufika ukingoni, alipanda basi na kwenda katiak madhabahu ya Mama Bikira Maria ya Lulijan, umbali wa 70 km mbali, ambako alisali na kumlilia Mungu ayaokoe maisha ya mwanae na Mungu alisikia sala yake na aliporejea nyumbani alimkuta mtoto wake akiwa amepona. :

Papa alihitimisha homilia yake akisema tunahitaji kuomba kwa moyo wa imani na ushujaa zaidi kwamba Mungu anaweza kila jambo. Hakuna anayeweza kusema ni peke yake ni jasiri wa maombi, bali kila mmoja ni jasiri, kinachotakiwa ni kuwa na Imani kwa Bwana. Papa alieleza na kuwataka wote watoleee sala zao kwa imani thabiti kwa ajili ya watu wengi ambao wanakabiliwa katika vita, wakimbizi wote na wote wnaokabiliwa na hali ngumu za maisha zilizo nje ya uwezo wao akisemam twapaswa kusema, Bwana, naamini na msaada wangu utatoka kwako leo hii. .








All the contents on this site are copyrighted ©.