2013-05-18 11:10:38

Sensa ya watu na makazi inafanyika kwa mara ya kwanza nchini Angola tangu ilipojipatia uhuru wake! Inagharimiwa na Angola yenyewe!


Nchi ya Angola, kwa mara ya kwanza imeanza kufanya sensa ya watu na makazi tangu ilipojipatia uhuru wake. Mara ya mwisho Angola ilifanya sensa ya watu na makazi kunako mwaka 1973 miaka miwili kabla ya kujipatia uhuru wa bendera, lakini baada ya muda mfupi, Angola ilijikuta ikingia kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo kwa takribani miaka ishirini imekuwa ni kikwazo kikubwa cha ustawi na maendeleo ya wananchi wa Angola.

Umoja wa Mataifa, Brazil, Cape Verde na Msumbiji zitatoa msaada wa kiufundi ili kufanikisha zoezi hili. Serikali ya Angola inakadiria kwamba, gharama ya sensa na makazi ya watu nchini humo itagharimu kiasi cha dolla za kimarekani Millioni 73 sawa na kiasi cha Billioni 7 za Kwanza ambayo ni fedha ya Angola.

Hayo yamebainishwa na Bwana Camilo Ceita, Mkurugenzi wa Taasisi ya Takwimu nchini Angola na kukazia kwamba, Angola ni kati ya nchi chache sana Barani Afrika ambazo zinaendesha sensa ya watu na makazi kwa kutumia fedha yake bila kuhitaji msaada wa wafadhili kutoka nje ya nchi.







All the contents on this site are copyrighted ©.