2013-05-17 08:38:09

Wito na utume wa Masista wa Kazi ya Roho Mtakatifu


Mheshimiwa Sr. Maria Eugenia Thomas, Mama Mkuu wa Shirika la Masista wa Kazi ya Roho Mtakatifu katika mahojiano na Radio Vatican anabainisha kwamba, wao kama Shirika wana utume wa kuendeleza kazi ya Yesu Kristo Mfufuka aliyemtuma Roho Mtakatifu ili kuendeleza ile kazi iliyokuwa imeanzishwa na Yesu kwa kuwakumbusha waamini yale yaliyofundishwa na Yesu pamoja na kuwafunulia ukweli wote. RealAudioMP3

Kama Masista wa Kazi ya Roho Mtakatifu wanatumwa kupeleka upendo wa Mungu aliyejifanya mwanadamu, hivyo wanapaswa kusikiliza kwa makini na kufuata maongozi ya Roho Mtakatifu, ili kusoma alama za nyakati na kutenda kadiri ya mahitaji ya watu wa nyakati hizi. Lengo ni kupata Pentekoste Mpya ambayo Mwenyezi Mungu atakuwa yote katika yote. Hii inamaanisha kuleta mabadiliko katika maisha ya mtu mzima: kiroho na kimwili.

Hii ni changamoto kwa kila mtu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, kushiriki katika mchakato unaopania kumletea mwanadamu maendeleo endelevu kwa kusoma alama za nyakati sanjari na utunzaji wa mazingira na mafao ya wengi. Masista wa Kazi ya Roho Mtakatifu wanatumwa kuwa ni vyombo vya haki, amani, upendo na mshikamano kama sehemu ya mchakato wa kumwendeleza mtu mzima.







All the contents on this site are copyrighted ©.