Padre Adolfo Nicolàs, SJ, achaguliwa kuwa ni Rais wa Mashirika ya Kitawa na Kazi za
Kitume Duniani
Askofu mkuu mteule Josè Rodriguez Carballo, Katibu mkuu wa Baraza la Kipapa la Mashirika
ya Kitawa na Kazi za Kitume ametuma salam za pongezi kwa Mheshimiwa Padre Adolfo Nicolàs,
S.J. Mkuu wa Shirika la Wayesuit kwa kuchaguliwa kwake kuwa Rais wa Shirikisho la
Mashirika ya Kitawa na Kazi za Kitume Duniani.
Kabla ya uteuzi huu, Padre
Nicolàs alikuwa ni Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mashirika ya Kitawa na Kazi za
Kitume. Nafasi hii inatarajiwa kujazwa wakati wa mkutano mkuu utakaofanyika mwezi
Novemba 2013.