2013-05-16 10:47:27

Watanzania wanaoishi Roma kusali kwa ajili ya kuombea amani, umoja na mshikamano wa kitaifa hapo Jumamosi, tarehe 18 Mei 2013


Watanzania wanaosoma na kuishi Roma, Jumamosi tarehe 18 Mei 2013 wataadhimisha Ibada ya Misa takatifu kwa ajili ya kuombea amani, upendo na mshikamano miongoni mwa watanzania wakati huu Tanzania inapopitia kipindi cha hali ya wasi wasi na majonzi makuu kutokana na vurugu za kidini. Hii itakuwa ni fursa pia kwa watanzania kusherehekea umoja na mshikamano wao wa kitaifa. Ibada hii itafanyika kwenye Chuo cha Kipapa cha Mtakatifu Petro, mjini Roma.

Taarifa iliyotolewa na viongozi wa wanafunzi watanzania wanaosoma Roma inaonesha kwamba, watanzania watatumia nafasi hii pia kuwaaga wale ambao wamehitimu masomo yao katika nafasi mbali mbali na sasa wako tayari kurudi Tanzania kuendelea kujenga Kanisa na Nchi kwa ujumla. Itakumbukwa kwamba, hii pia ni nafasi kwa ajili ya kuwapongeza watanzania waliopiga hatua mbali mbali katika maisha ya wito wao kama Makleri na Watawa.







All the contents on this site are copyrighted ©.