2013-05-16 11:13:03

Papa Francisko kutembelea Cagliari, Septemba 2013


Baba Mtakatifu Francisko wakati akitoa Katekesi yake kwa mahujaji na wageni waliokuwa wamemiminika kwa wingi kwenye Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Petro mjini Vatican, jumatano iliyopita ameonesha nia ya kutaka kutembelea Madhabahu ya Bikira Maria wa Bonaria yaliyoko Kisiwani Sardenia, mjini Cagliari nchini Italia na kwamba, kama hakutakuwepo na kizuizi chochote basi, hija hii ya maisha ya kiroho angependa kuifanya Mwezi Septemba 2013. Hii ni kutokana na uhusiano wa kidugu na wa muda mrefu uliopo baina ya miji ya Buenos Aires na Cagliari.

Mji wa Bueonos Aires ulipoanzishwa ulijulikana kama mji wa Fumbo la Utatu Mtakatifu, lakini Mabaharia walipofika mjini hapo wakabadili jina na kuita mji wa "Madonna wa Bonaria". Jina linalotumika hadi leo hii.







All the contents on this site are copyrighted ©.