Kardinali Keith Patrick O'Brien, Askofu mkuu mstaafu wa St. Andrews na Edinburgh nchini
Scotland kutokana na sababu zilizopelekea kushindwa kwake kuhudhuria Conclave na kwa
makubaliano na Vatican, ameamua kwa miezi kadhaa kutoka nchini Scotland na kwenda
"Jangwani" kwa ajili ya mafungo ya maisha ya kiroho, sala na toba. Maamuzi na mipango
mingine kwa ajili ya Kardinali O'Brien itapangwa kwa makubaliano na Vatican.