Taasisi za fedha katika kudumisha mafao ya wengi na maadili katika Jamii
Baraza la Kipapa la haki na amani kwa kushirikiana na Benki pamoja na taasisi za fedha
na wafanyabiashara wa Kikristo, wameanza majadiliano kuhusu mfumo wa Benki kwa ajili
ya mafao ya wengi pamoja na maadili yanayopaswa kuzingatiwa na taasisi za fedha wakati
wa kutekeleza majukumu yake ndani ya Jamii husika.
Mkutano huu umefunguliwa
rasmi siku ya Jumatatu na Kardinali Peter Turkson, Rais wa Baraza la Kipapa la haki
na amani na unatarajiwa kuhitimishwa hapo tarehe 14 Mei 2013.