2013-05-11 15:40:43

SECAM yaanzisha Shirika la Habari za Afrika


Shirikisho la Mabaraza ya Maaskofu Katoliki Afrika na Madagascar, SECAM, kuanzia tarehe 2 Mei 2013 limeanzisha Shirika la Habari la SECAM na kumteua Don Bosco Ochieng Onyalla kutoka Jimbo Katoliki la Rumbek, Sudan ya Kusini kuwa mkurugenzi wake wa kwanza. Makao makuu ya Shirika hili litakalojulikana kama Catholic News Agency fo Africa, CANAA yatakuwa Jijini Nairobi, Kenya.

Padre Onyalla amepewa dhamana ya kuanzisha ofisi za habari kwa kushirikiana na Askofu mkuu Chrles G. Palmer Buckle wa Jimbo kuu la Accra, Ghana ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Bodi ya CANAA. Padre Onyalla atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kwamba, anawasiliana na wadau mbali mbali wa habari kutoka ndani na nje ya Bara la Afrika, ili kuunga mkono jitihada za kukuza na kuendeleza mawasiliano ya jamii kama sehemu ya mchakato wa Uinjilishaji Mpya na ule wa kina.

Padre Onyalla alikuwa ni mwanzilishi wa Radio Good News ya Jimbo Katoliki Rumbek hadi mwezi Oktoba 2012.







All the contents on this site are copyrighted ©.