2013-05-11 08:26:56

Ripoti ya nne juu ya hali ya uhai wa Mafundisho Jamii ya Kanisa imewasilishwa.


Alhamis , katika Makao Makuu ya Mafundisho Jamii ya Kanisa Ulimwenguni, kuliwasilishwa "Ripoti ya Nne juu ya hali ya Uhai wa Mafundisho Jamii ya Kanisa ulimwengu".
Ripoti hiyo imetolewa na Mtazamji wa Kimataifa Shirika la Van Thuan , kwa kushirikiana na Kikundi cha Kitume cha Kikristu (MCL). Na wametazama zaidi, hoja nzito za kimaadili zisizokuwa na mbadala: maisha, familia, uhuru, amani na haki ya kijamii. Na Miongoni mwa hoja za kidharura zinazo nyambuliwa zaidi kwa mwaka huu ni ukolonishaji wa asili ya binadamu, matokeo yake katika upanuzi wa maendeleo ya kile kinachojulikana “itikadi jinsia.”

Askofu Giampaolo Crepaldi, Askofu Mkuu wa Trieste na Rais wa Van Thuan, katika maelezo yake ya wakati wa kuiwasilisha ripoti hiyo amesema, kinachohitajika zaidi katika hoja hii ya itikadi za kijenda, zilizoanzishwa kwa kasi kubwa barani Ulaya na kuenea haraka katika mataifa mengine, ya Ulaya , nchi zingine kama vile Argentina, ni kutokwenda kinyume na utu wa biandamu na mwelekeo wa maisha adilifu na maisha ya familia.

Alitaja Mienendo inayo jaribu kuharibu tendo la ndoa, na binadamu kuwekwa katika hatari ya kudharirisha utu wake, imekuwa ni changamoto kwa Kanisa, kufufua thamani ya "sheria ya asili" kama kituo rejea katika utoaji wa maoni na Uinjilishaji Mpya.

Askofu Mkuu Cleopaldi ameasa juu ya dhania kwamba, hali hizi halisi, na taratibu hizi kitamaduni, kisiasa na kijamii, hudhoofisha imani. Lakini yeye ana imani kwamba, imani hukomaa zaidi kwa kupambana na changamoto. Na hivyo hali hiyo hulazimu imani kujenga taratibu ambazo matokeo yake ni kuyabatilisha yale ya kibinadamu.
Ni hivyo inakuwa dhahiri kwamba, jibu katika masuala haya ya imani , linapaswa kuwa lile lenye wa kuiamusha imani , na hasa kanisa kuondokana na kuhofia mapambano, badala yake, changamoto zinakuwa ni mwanya mzuri wa kuushuhudia ukweli kwa kutoa majibu ya kuaminika, na kushawishi.
Kwa maana hiyo, utume uliofumbatwa katika Mafundisho Jamii ya Kanisa ni kutetea vyema nafasi kanisa katika umma, hasa thamani ya maisha ya binadamu na viumbe na tunu za maisha zisizokuwa na mbadala.









All the contents on this site are copyrighted ©.