Papa Fransisko: Kanisa ni Unyenyekevu, Ujasiri, Uwazi na njia ya wote
Wachambuzi wa mahubiri ya Papa , wakitazama mafundisho ya Papa Frasisko, tangu achaguliwe
kuwa Papa, ikiwa zimebaki siku chache kutimia miezi miwili kamili wanasema, ujumbe
wake katika mahubiri anayoyatoa kila siku asubuhi katika Ibada anazo ziongoza katika
Kikanisa cha Mtakatifu Marta kila siku asubuhi, ni juu ya tabia na utambulisho wa
Kanisa, ambao ni kielelezo cha unyenyekevu na moyo wa shujaa katika kumsikiliza Roho
Mtakatifu. Hili limebainishwa na Gazeti la L’Osservatore Romano, ambamo mna maeelzo
kwamba Papa Fransisko, amefanya rejea nyingi katika kitabu cha Matendo ya Mitume
, juu ya maisha ya jamii ya kwanza ya Kikristo ya Yerusalemu, akitazama kwa makini
utambulisho wa kanisa na utume tangu mwanzo wa Kanisa.
Maelezo yake yanalitaja
kanisa kuwa ni unyenyekevu na ushupavu, wa kuisikiliza Roho Mtakatifu, na ambalo
hutoka nje lenyewe kwa ushupavu, kwenda katika kila pembe ya dunia, kwa nia ya kuhubiri
kile linacho kiamini, Injili ya Upendo wa Yesu Kristu, aliyesulubiwa kufa na kufufuka
katika wafu kwa ajili ya kumkomboa binadamu. Kwamba Kanisa ni mama, na si yaya.
Kanisa hujenga madaraja ya upendo kati ya watu, huwakutanisha na si kuejnga kuta
za kutenganisha watu. Milango ya Kanisa ni wazi, likijulikana kama ni jumuiya ya
upendo na si kama ni shirika au chama cha kujitegemea au NGO. Katika kipindi
hiki cha chini ya miezi miwili, Papa Francisko ametoa tafakari nyingi kwa waamini,
kwa lugha nyepesi lakini yenye kutoa maana ya kina, juu ya maana ya kuishi ndani ya
Kanisa, na maana ya kuwa msharika wa Kanisa. Daima anakumbusha kwamba, kwanza zaidi
ya yote, kila mbatizwa, anawajibika kuliendeleza Kanisa. Kumtangaza Kristo, akiwa
kweli Mkristo hai katika imani, na si kama wakili, bali mhusika kamili, aliyepokea
zawadi ya ubatizo, inayotufanya kusonga mbele kwa nguvu za Roho Mtakatifu, katika
kumtangaza Yesu Kristo. Hiyo ndiyo maana kuwa Mkristu. Daima ni kutembea katika
njia hii ya imani bila kusimama. Papa Francisko anaasa, pale Kanisa linapopoteza
ujasiri huu, wa kuitangaza Injili ya Kristu, kanisa hilo hupoteza umotomoto wa roho
wake na hivyo kuwa na ubaridi. Ubaridi huo, huliumiza Kanisa kwa kiasi kikubwa ,
kwa sababu, hurudisha nyuma asili ya utendaji wake, na hivyo ndani mwake mnazuka
matatizo kati ya Waaamini, na kuupoteza mwelekeo jasiri wa imani na sala za kuelekea
mbinguni, ujasiri wa kutangaza Injili. Papa Francisko, hata hivyo anaonya , ujasiri
huo, tunauona t, kwa kupata uelewa wa kulipokea Neno la Mungu kwa moyo wa unyenyekevu
, na utulivu wa moyo, na kutompinga Roho Mtakatifu. Na hivyo ndani ya Kanisa, tunapata
maana ya kuwa kweli jumuiya halisi, inayodumu katika upendo wa Kristo.
Papa
Francisko amekuwa akiasa, Sisi, waamini wa kanisa , wanawake kwa wanaume tuliyomo
ndani ya Kanisa, ni sehemu ya historia hii ya upendo , kila mmoja wetu ni kiungo katika
mnyororo wa upendo . Kama hili hatulielewi , kamwe hatuwezi kuelewa Kanisa ni kitu
gani.
Papa pia amekuwa akionya juu ya hatari za kujitenga mbali na kanisa
,hasa wakati wa misukosuko na majaribu ya kujenga Kanisa katika kipimo chetu. Mara
kwa mara anarudia kusisitiza kwamba, Njia ya Yesu si itikadi na uzushi unaotafuta
faida binafsi , lakini ni njia inayo onyesha mwelekeo wa kweli, hasa pale linapokabiliwa
na dhoruba za matatizo na majaribu. Pale linapo shinikizwa na itikadi za malimwengu,
au pale roho wa malimwengu anaposhinikizwa ndani mwake na imani isiyo toka kwa Bwana
na madhaifu mengine yaliyo lifanya kanisa kupoteza onjo lake la kuwa mshindi dhidi
ya mambo ya kilimwengu. Waamini wanapaswa kukumbuka Kanisa lisilokuwa ujasiri
wa ushindi wa Injili, ushindi wa kuupeleka ujumbe wa Injili ya Msalaba,na kashfa
ya Msalaba kwa watu wote, haliweza kusonga mbele katika kupambana na malimwengu. Na
hivyo huingia katika hatari za kurudi nyuma.