2013-05-10 10:09:36

Billioni 1.36 za pato la DRC zimepotea katika mazingira ya kutatanisha!


DRC katika kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi mwaka 2012 imepoteza mapato kiasi cha dolla za kimarekani zipatazo billioni 1.36 kutokana na zoezi la kupunguza mauzo kwa baadhi ya Makampuni ya uchimbaji wa madini nchini humo, kadiri ya taarifa iliyotolewa na Jopo linaloongozwa na Kofi Annan, aliyekuwa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa katika Jukwaa la Uchumi wa Afrika. Upotevu huu wa fedha ni sawa na bajeti iliyotolewa na DRC kwa ajili ya Wizara ya Afya na Elimu kwa Mwaka 2012.

Taarifa hii inaonesha jinsi ambavyo rasilimali na utajiri wa wa Bara la Afrika unavyokwapuliwa na wajanja wasiozingatia utawala wa sheria, mafao ya wengi wala uzalendo kwa nchi yao. Kutokana na hali hii kuna haja ya kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini mahali ambapo fedha hizi zimetokomea kwa kuyahusisha makampuni yanayojishughulisha na uchimbaji wa nishati na madini nchini DRC. Jopo hili linasema kwamba, hizi ni dalili za rushwa, ufisadi na ukosefu wa misingi ya ukweli na uwazi.







All the contents on this site are copyrighted ©.