Roho Mtakatifu anawakirimia waamini imani katika upendo na huruma ya Mungu!
Baba Mtakatifu Francisko anawaambia watumiaji wa mitandao ya kijamii kwamba, zawadi
kubwa ambayo Roho Mtakatifu wanawaletea waamini ni ile ya kutumainia upendo na huruma
ya Mungu. Kwa Siku kuu ya Kupaa Bwana kwenda mbinguni, waamini wanaanza kipindi cha
Novena kama sehemu ya mchakato wa kujiandaa kwa ajili ya ujio wa Roho Mtakatifu.