Nyongeza ya mishahara ya Wabunge yawachefua wananchi wa Kenya
Kardinali John Njue, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Kenya ameonya mwelekeo wa
Wabunge wa Kenya kutaka kuongezewa mishahara kwamba, si wazo jema kwa wakati huu ambapo
watu wengi wanaendelea kuathirika kutokana na myumbo wa uchumi kimataifa.
Nyongeza
ya mishahara ya wabunge itakuwa na athari kubwa kwa uchumi wa nchi ya Kenya ambao
bado unaendelea kusua sua. Kardinali Njue anasema kuna mambo ambayo kwa sasa yanapaswa
kupewa kipaumbele cha kwanza na wala si nyongeza ya mishahara ya Wabunge.
Watu
wa kawaida wanapaswa kufikiriwa kwanza kabla ya kuanza mchakato wa nyongeza ya mishahara
ya wabunge anasema Kardinali John Njue. Taarifa kutoka Kenya zinabainisha kwamba,
Bunge la Kumi na Moja tangu lilipoanza kikao chake limejielekeza zaidi kutaka kuongezewa
mishahara na kufutiwa kodi, mawazo ambayo yamewachefua wananchi wengi wa Kenya.