2013-05-08 15:25:10

Mungu anatupenda kama Baba - Papa Fransisko


Mafundisho ya Papa Fransisko kwa mahujaji na wageni Jumatano hii yanasema, katika kipindi hiki cha maadhimisho ya Pasaka, kipindi tunachokiishi kwa furaha, tukiongozwa na Liturujia ya Kanisa,tunaiishi furaha kamili ya Roho Mtakatifu tuliyopewa na isiyokuwa na kipimo na aliyesulibiwa na kufufuka Yesu Kristu (Yn3:34). Huu ni wakati wa neema unaokamilika kwa Sikukuu ya Pentekoste, wakati Kanisa linauishi upya uzoefu wa kumiminwa kwa mwanga kwa Roho juu ya Maria na Mitume wa Yesu , walipokusanyika katika maombi kwenye chumba cha juu ghorofani.

Papa Fransisko amehoja ni nani Roho Mtakatifu? na kutoa jibu kwa kuirejea sala ya Nasadiki, ambayo Mkristu huikiri imani yake akisema, "Naamini katika Roho Mtakatifu, Bwana na mtoaji wa uzima".

Papa amefafanua., huu ni ukweli wa kwanza ambao kila Mkristu huuzingatia wakati wa kukiri Imani yake, ni kwamba Roho Mtakatifu ni Bwana. Hii ina maana kwamba Yeye ni Mungu kweli kama ilivyo Baba na Mwana, na kwamba sisi tunapomkiri Roho Mtakatifu tunamuunganishwa moja kwa moja na Baba na Mwana. Roho Mtakatifu, ni kweli, nafsi ya tatu ya Utatu Mtakatifu, Roho Mtakatifu ambaye ni zawadi kubwa ya Kristo Mfufuka, aliye mfunua katika akili zetu na mioyo yetu kupitia imani kwa Yesu, kuwa ni Mwana aliyetumwa kutoka kwa Baba, ambaye hutuongoza katika urafiki, na kutuunganisha katika ushirika na Mungu

Papa aliendelea kuangalisha katika ukweli kwamba Roho Mtakatifu ni chanzo kisichokuwa na mwisho cha maisha ya kimungu ndani wetu. Katika nyakati zote na kwa kila mtu, mna hamu ya kutaka kuwa na maisha makamilifu mazuri, maisha ya haki na wema, maisha ambayo si ya kutishiwa na kifo, lakini ambayo yamaweza kukomaa na kukua katika ukamilifu wake.
Papa ameendelea kumweleza mtu kama ni msafiri anayevuka jangwa la maisha, ana kiu ya maji yaliyo hai, maji yanayo miminika na safi, yenye uwezo wa kuzima hamu yake ya kina katika kuupata mwanga wa uzuri wa upendo, na amani. Na kwamba sisi wote, huisikia hamu hii. Na Yesu yuko tayari kutupatia maji yaliyo hai: ambaye ni Roho Mtakatifu, atokaye kwa Baba na Mwana, Roho anayemiminwa katika mioyo yetu. Yesu anatuambia kwamba "Nimekuja ili wawe na uzima na kuwa ni uzima kamili" (Yohana 10, 10).








All the contents on this site are copyrighted ©.